ZAA YAKANUSHA TAARIFA ZA WIZI WA MIZIGO UWANJA WA NDEGE WA (AAKIA)

Zanzibar, 11 Februari 2026 Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Zanzibar (ZAA), Ndugu Seif Abdalla Juma, ametoa ufafanuzi kwa umma kufuatia taarifa zilizosambazwa kwenye baadhi ya mitandao ya kijamii na vyombo vya habari zikidai kuwa mamlaka hiyo imeshindwa kudhibiti matukio ya wizi wa mizigo katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume (AAKIA).

WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AFUNGUA UWANJA WA NDEGE WA MTEMERE

Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba leo Februari 11, 2026 amezindua uwanja wa ndege Mtemere uliopo katika kijiji cha Mloka, mkoani Pwani kwenye hifadhi ya Taifa ya Nyerere.

Uzinduzi wa uwanja huo umeenda sambamba na uzinduzi wa miradi mingine 20 (kufanya miradi 21) ikiwemo Malango ya kuingilia Hifadhini, vituo vya taarifa kwa wageni, kambi za wageni, Eneo la Kupumzikia wageni, Nyumba za wageni, Hosteli za Wanafunzi, kituo cha kufuatilia ikolojia, na vituo vya askari.

Subscribe to
 

Simplenews subscription

The subscriber's email address.
Stay informed - subscribe to our newsletter.