MO, DEWJI AMHOJI MANGUNGU MTANDAONI KUHUSU MABADILIKO YA KLABU YA SIMBA

Mwekezaji wa klabu ya Simba na Mfanyabiashara Mohammed Dewij ameibuka Mtandao na kuhoji hatua iliyofikiwa katika mchakato wa Mabadiliko ya Mfumo wa uendeshaji wa Klabu ya Simba.

Swali hilo limeibuka wakati Uongozi wa klabu ukitangaza rasmi kurejesha usajili wa wanachama kwenye mkutano wake na Vyombo vya Habari Jijini Dar es Salaam. Leo Februari 10,2026.

NDANI YA SIKU 100 WIZARA TUMEFANIKIWA KUTOA AJIRA 2,300

Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya Zanzibar, Dkt. Mngereza Mzee Miraji, ameeleza utekelezaji wa majukumu ya Wizara ya Afya kuanzia ngazi ya msingi hadi ngazi ya juu ya rufaa, ikiwa ni sehemu ya kuimarisha mfumo wa huduma za afya Zanzibar.

Ndani ya siku 100 za utekelezaji, Wizara imefanikiwa kuajiri wahudumu wa afya ngazi ya jamii 2,300, hatua iliyopanua upatikanaji wa huduma za afya mashinani, sambamba na kuhakikisha mishahara inalipwa kwa wakati kutokana na uongozi na maelekezo ya Mheshimiwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Ali Mwinyi.

SMZ IMEFANYA MAPINDUZI MAKUBWA KWENYE SEKTA YA AFYA

Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya Zanzibar, Dkt. Mngereza Mzee Miraji, ameeleza kwa kina dira ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Ali Mwinyi, ya kuiondoa Zanzibar katika utegemezi wa rufaa za matibabu nje ya nchi na badala yake kuijenga kuwa kitovu muhimu cha huduma za afya katika ukanda wa Afrika Mashariki.

ZANZIBAR INAENDELEA KUPIGA HATUA KWENYE SEKTA YA UTALII KIMATAIFA

Katibu Mkuu wa Wizara ya Utalii na Mambo ya Kale, Dkt. Aboud Suleiman Jumbe Akizungumza katika tathmini ya utekelezaji wa siku 100, amesema Zanzibar imeendelea kufanya vizuri na kujipatia nafasi kwenye orodha mbalimbali za kimataifa za utalii.

Ameeleza kuwa Zanzibar sasa ipo katika kumi bora barani Afrika kwenye vivutio vya utalii, miradi bora ya kitalii, maeneo bora ya honeymoon pamoja na michezo ya baharini, hali inayoongeza ushindani na kuimarisha nafasi ya Zanzibar katika soko la kimataifa la utalii.

ZANZIBAR SEKTA YA UTALII INAKUA KWA KASI, ZAIDI YA WATALII LAKI 1 WANATEMBELEA KWA MWEZI

Baada ya kuapishwa kwa Mhe. Rais  Dkt. Hussein Mwinyi kuongoza Zanzibar katika awamu ya nane ya uongozi, sekta ya utalii imeonesha ukuaji mkubwa na wa kasi. Katika mwezi wa kwanza wa uongozi huo, idadi ya watalii ilikuwa takribani elfu 72 pekee.
Hata hivyo, kwa sasa kuanzia Novemba hadi Januari, Zanzibar inapokea wastani wa watalii laki 1 kwa kila mwezi.

Subscribe to
 

Simplenews subscription

The subscriber's email address.
Stay informed - subscribe to our newsletter.