WAZIRI MKUU ACHUKIZWA NA MIGOGORO YA ARDHI

WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba amewasisitiza Mawaziri, Wakuu wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya pamoja na watumishi wa umma wahakikishe wanatenga muda wa kusikiliza na kutatua kero za wananchi katika maeneo yao hususani kwenye migogoro ya ardhi katika ngazi zao za kiutawala. 
 
Ameyasema hayo leo Ijumaa, Februari 6, 2026 wakati wa kuahirisha Mkutano wa Pili wa Bunge la 13 jijini Dodoma, akisisitiza kuwa viongozi hao wanapaswa kuwafuata wananchi, kuwasikiliza na kuchukua hatua za haraka za kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili wakiwa katika maeneo yao.

DKT. MWINYI KUFUNGUA IJTIMAI ZANZIBAR

Rais Wa Zanzibar Na Mwenyekiti Wa Baraza La Mapinduzi, Alhaj Dkt. Hussein Ali Mwinyi, Kesho Anatarajiwa Kuwa Mgeni Rasmi Katika Ufunguzi Wa Ijtimai Ya Kimataifa Itakayofanyika Katika Eneo La Fuoni Migombani.

Maandalizi Ya Ijitimai Hiyo Tayari Yamekamili Huku Waumini Wa Dini Ya Kiislamu Wakihimizwa Kuhudhuria Katika Ijitimai Hiyo Ambayo Itawakumbusha Mambo Ya Heri Na Kumcha Mwenyezi Mungu.

WADAU WA USALAMA BARABARANI WATAKIWA KUSHIRIKIANA

Mkuu Wa Mkoa Wa Mjini Magharibi, Moh’d Abdalla Ali, Amesema Wafanyabiashara Wa Soko La Mombasa Wanatarajiwa Kuanza Kufanya Biashara Zao Ndani Ya Soko Hilo Katika Kipindi Cha Hivi Karibuni.

Akizungumza Na Waandishi Wa Habari, Mheshimiwa Mohd Abdalla Ali Amesema Tayari Wameshagawa Vizimba Kwa  Wafanya Biashara Na Wanatarajia Kuanza Kulitumia Soko  Kabla Ya Mwezi Wa Ramadhani

ZBC YATUNUKU ZAWADI KWA WAFANYAKAZI BORA

Mwenyekiti Wa Bodi Ya Shirika La Utangazaji Zanzibar Zbc Mhandisi Idrisa Muslim Hijja Amesema Ili Kufikia Dhamira Ya Serikali Kuimarisha  Maendeleo Ni Muhimu Kwa Wafanyakazi Kujituma Zaidi Katika Kutekeleza Majukumu Yao

 

Akizungumza Katika Hafla Ya Kuwapongeza Wafanyakazi Wa Shirika Za Utangazaji Zbc Waliofanya Vizuri Kwa Mwaka Huu Kupitia Hafla Maalum Ya Utoaji Tuzo Amesema Hatua Inalenga Kuimarisha Uwajibikaji ,Ubunifu Na Kuongeza Motisha Katika Kufanya Kazi

Subscribe to
 

Simplenews subscription

The subscriber's email address.
Stay informed - subscribe to our newsletter.