MADIWANI MBULU WATAKA WASIOCHANGIA CHAKULA SHULENI WACHUKULIWE HATUA

Baraza la madiwani wa halmashauri ya mji wa Mbulu mkoani Manyara wameiomba Serikali  kuwachukulia hatua kali za kisheria Wazazi wasiochangia chakula kwa watoto wao shuleni ili kuwezesha watoto kupata chakula cha mchana na kuinua kiwango cha taaluma.


Madiwani hao Wametoa Ombi hilo wakati wa kikao cha kwanza cha baraza hilo ambapo wamelalamikia tabia ya baadhi ya wazazi kutochangia mchango wa chakula shuleni kwa watoto wao hali inayokuwa kikwazo kwa jitihada za kuinua taaluma na kuondokana na utoro shuleni.

MAHAKAMA YAPENI KIPAUMBELE MASHTAKA YA UKATILI DC KAGANDA.

Serikali Mkoani Manyara imeishauri mahakama kuyapa kipaombele mashauri yanayohusu ukatili wa kijinsia na kutoa adhabu yenye kuleta majuto kwa jamii na wanaohusika na matukio hayo.


Kauli hiyo kwa mahakama Kanda ya Manyara imetolewa na Mkuu wa wilaya ya Babati Emanuela Kaganda kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Manyara Queen Sendiga wakati akizungumza kwenye maadhimisho ya siku ya sheria Nchini yaliyofanyika kwenye viwanja vya mahakama hiyo Mkoani humo.

ZANZIBAR YASAINI MRADI WA KUIMARISHA MIUNDOMBINU

Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imesaini Mkataba wa Miaka Mitano na Czech–Tanzania Development Chamber of Commerce, unaolenga kuimarisha miundombinu na kuchochea uchumi endelevu wa Zanzibar. 

Miongoni mwa Maeneo yatakayotekelezwa ni Sekta ya usafiri wa Anga na Barabara ya Reli na Miradi mingine ya kimkakati ili kuongeza fursa za kiuchumi. 

MAFUNZO YA UTUMISHI KWA WAFANYAKAZI NI MUHIMU KAZINI

Kaimu Mkurugenzi wa Kampuni inayotoa huduma za bima zinazozingatia misingi na sharia ZIC Takaful Ndg.Said Abdallah Basleym amesema suala la Mafunzo kwa Wafanyakazi ni jambo la kupewa kipaumbele ili kuhakikisha wanaendana na kasi ya utendaji na kufanya kazi kwa ufanisi zaidi.

Akizungumza wakati wa Mafunzo ya kujenga uwezo yaliyotolewa kwa Wafanyakazi wa Kampuni hiyo, Ndg. Said ameeleza kuwa uwekezaji katika Mafunzo husaidia kuongeza ufanisi katika utendaji kazi wa Kampuni, pamoja na kuboresha huduma zinazotolewa kwa Wananchi.

Subscribe to
 

Simplenews subscription

The subscriber's email address.
Stay informed - subscribe to our newsletter.