WATATU WATHIBITISHWA KUWA WENYEVITI WA BUNGE

Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania leo limewathibitisha Wabunge Deo Mnyika, Cecilia Pareso na Nagma Murtaza Giga kuwa Wenyeviti wa Bunge hilo .

Hayo yamejiri baada ya Spika wa Bunge Mussa Azzan Zungu kuwahoji Wabunge kikanuni kama waanafiki Wabunge hao kuwa Wenyeviti wa Bunge.

Wabunge hao waliteuliwa na Kamati kuu ya Chama cha Mapinduzi CCM kilichoongozwa na Mwenyekiti wa Chama hicho Dkt.Samia Suluhu Hassan January 25 Mwaka huu Mjini Zanzibar.

KILIO CHA SHERIA YA HABARI ZANZIBAR CHAIBULIWA UPYA

Wadau wa Vyombo vya Habari Nchini wameibua tena kilio chao cha kupatikana kwa sheria ya habari hapa Zanzibar na kwa kauli moja wameitaka Wizara ya Habari, Sanaa Utamaduni na Michezo kuhakikisha wanaikata kiu yao ya muda mrefu ya kuipata sheria hii.

Huu ulikuwa ni Mkutano mahususi kati ya Wizara ya Habari, Sanaa Utamaduni na Michezo na Wadau wa Sekta ya Habari ukiwa na lengo la kupata maoni, ushauri kero na mjadala wa kujenga uhuasiano mwema kati ya Sekta ya Habari na Wadau wake.

MAMA SAMIA NI KIONGOZI WA MFANO WA MAENDEELEO

Akinamama waliojifungua katika Hospital ya Wilaya Vitongoji Chake Chake Kituo cha Afya Kendwa na Tundauwa, wamesema Dkt. Samia ni Kiongozi imara na mwenye maono makubwa katika kuileta Nchi maendeleo.

Akinamama hao wameyasema hayo kwa nyakati tofauti mara baada ya kupokea zawadi kutoka  Ofisi ya CCM uratibu Pemba kwa akina mama hao

Waliyojifungua ikiwa ni kusherekea Siku ya Kuzaliwa ya Rais wa Jamuhuri ya Muungano  wa Tanzania Mama Samia Suluhu Hassan .

Subscribe to
 

Simplenews subscription

The subscriber's email address.
Stay informed - subscribe to our newsletter.