AJALI YA BASI NA LORI YAUA MMOJA NA KUJERUHI 12 SHINYANGA

Basi la Kampuni ya Kisire limegongana uso kwa uso na lori katika eneo la mnada wa Tinde Wilaya ya Shinyanga na kusababisha kifo cha mtu mmoja huku wengine 12 wakijeruhiwa na kukimbizwa Kituo cha afya Tinde kupata matibabu.

Ajali hiyo imehusisha basi la Kisire lenye namba za usajili T 229 EEL, lililokuwa likitoka Kahama kuelekea Mwanza, kugongana uso kwa uso na lori la mizigo lenye namba za usajili RAE 849N. lililokuwa limebeba shehena ya mchele kutoka Dar es Salaam kwenda nchi jirani ya Rwanda huku chanzo kikielezwa kuwa ni mwendo kasi.

MWENYEKITI RAJABU, TANGA NDIO CHIMBUKO LA SOKA NCHINI

Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Tanga Rajabu Abdallah amesema mkoa huo ndio chimbuko la vilabu vya mpira nchini,hivyo wadau waunge mkono timu za eneo hilo ili kufufua ushindani uliokuwepo.

Akizungumza  wakati wa sherehe za kukabidhi basi kwaajili ya timu ya mpira wa miguu ya African Sports Club zilizofanyika makao makuu ya timu hiyo mwenyekiti Rajabu amesema timu hiyo na Coastal Union ushabiki wake ni zaidia ya Simba na Yanga.

RC TANGA ATOA AGIZO KWA WAKUU WA WILAYA KUHUSU WAMACHINGA

Mkuu wa mkoa wa Tanga Balozi Batilda Buriani amewaagiza wakuu wa wilaya zote za eneo hilo kuwatafutia maeneo ya uhakika wafanyabiashara ndogondogo maarufu kama Machinga,na katafuta sehemu ambayo watakaa bila changamoto

Akizungumza wakati akifunga maadhimisho ya wiki ya huduma za fedha kitaifa yaliofanyika mkoani Tanga katika viwanja vya shule ya sekondari usagara kwa wiki moja Jumatatu Januari 26,2026 Balozi Batilda amesema wafanyabiashara ndogondogo wanatakiwa kuwekwa sehemu  nzuri.

Subscribe to
 

Simplenews subscription

The subscriber's email address.
Stay informed - subscribe to our newsletter.