Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amesisitiza umuhimu wa kuendeleza utaratibu wa kuisoma, kuihifadhi na kuzingatia mafundisho ya Qur-ani Tukufu miongoni mwa Vijana ili kujenga kizazi chenye Maadili, hofu ya Mwenyezi Mungu na mchango mzuri katika Jamii.