Chama cha Mapinduzi,(CCM) Mkoa wa Tanga kimeagiza kufuatiliwa na kuthibitishwa vikundi vyote vya Vijana,Wanawake na wenye Ulemavu katika Jiji la Tanga,ili kuweza kujua uhalali wake.
Agizo hilo limetolewa na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Tanga Rajabu Abdallah wakati kukabidhi pikipiki katika vikundi vya Vijana katika eneo la Kirare jijini Tanga April Mosi,2026 na kumuagiza Mwenyekiti wa UVCCM mkoa afuatilia kujua uhalali wake.