MWENYEKITI WA CCM TANGA AAGIZA KUFUATILIWA VIKUNDI VILIVYOPEWA MIKOPO

Chama cha Mapinduzi,(CCM) Mkoa wa Tanga kimeagiza kufuatiliwa na kuthibitishwa vikundi vyote vya Vijana,Wanawake na wenye Ulemavu katika Jiji la Tanga,ili kuweza kujua uhalali wake.

Agizo hilo limetolewa na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Tanga Rajabu Abdallah wakati kukabidhi pikipiki katika vikundi vya Vijana katika eneo la Kirare jijini Tanga April Mosi,2026 na kumuagiza Mwenyekiti wa UVCCM mkoa afuatilia kujua uhalali wake.

MBULU MJI YAJIPANGA KUUPOKEA MWENGE WA UHURU 2026 KWA MAFANIKIO

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Mbulu Bi. Rehema Bwasi  jana Aprili 1, 2026 ameongoza kikao cha tathmini ya mapokezi ya Mwenge wa Uhuru 2025, akiwapongeza watumishi wote wa halmashauri hiyo kwa ushiriki wao mkubwa ulioleta mafanikio ya kihistoria.

MIUNDO MBINU BORA YA BARABARA NI CHACHU YA MAENDELEO

Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Zanzibar Dkt.Khalid Salum Mohamed amesema lengo la Serikali la kuendelea kujenga miundombinu ya Barabara ni kurahisisha shughuli za usafiri na usafirishaji kwa Wananchi na Taifa.

Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Dkt .Khalid Salum Mohamed akizungumza wakati wa Ziara ya kukagua vifaa vya ujenzi wa Barabara vya Kampuni ya CCECC amesema vifaa hivyo vimekuja wakati sahihi na vitarahisisha ujenzi wa Barabara za Mjini 

 

KITUO CHA UMEME IFAKARA CHACHOCHEA MAENDELEO KILOMBERO

Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imetumia shilingi bilioni 25 kujenga Kituo cha Kupoza Umeme 1x20MVA, 220/33kv pamoja na njia za kusambaza Umeme katika Wilaya ya Kilombero, hatua ambayo imeboresha upatikanaji wa umeme na kuondoa changamoto ya kukatika kwa nishati hiyo katika wilaya za Kilombero, Ulanga na Malinyi.

Subscribe to
 

Simplenews subscription

The subscriber's email address.
Stay informed - subscribe to our newsletter.