HARAKATI ZA KUKITAMBUA KISWAHILI MITANDAONI ZAANZA

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo wa Tanzania Paul Makonda, amesema Serikali imeanza mazungumzo na UNESCO pamoja na Uongozi wa Kampuni Mama inayomiliki Mitandao ya Kijamii ya Faceebok, Instagram na Whatsapp (Meta) ili lugha ya Kiswahili itambulike rasmi kwenye majukwaa ya Mitandao hiyo na kuwezesha Vijana wanaotengeneza maudhui kwa Lugha hiyo walipwe malipo makubwa kulingana na kazi zao.

Makonda ameyazungumza haya wakati wa Kongamano la 5 la Idhaa za kKswahili Duniani lililofanyika Jana Arusha.

ZRCP ELIMISHENI UMUHIMU WA MATOKEO YA TAFITI

Rais Wa Zanzibar Na Mwenyekiti Wa Baraza La Mapinduzi Dkt. Hussein Ali Mwinyi, Ameushauri Uongozi Wa Kituo Cha Tafiti Za Kiuchumi, Kijamii Na Uchambuzi Wa Sera Zanzibar –Zrcp- Kuandaa Mikutano Na Mijadala Na Wadau Ili Kuwaelimisha Kuhusu Umuhimu Wa Kutumia Matokeo Ya Tafiti Katika Utekelezaji Wa Majukumu Yao.

Ni Ziara Ya Ujumbe Wa Kituo Cha Tafiti Za Kiuchumi, Kijamii Na Uchambuzi Wa Sera Zanzibar –Zrcp- Katika Ikulu Ya Vuga Hapa Zanzibar.

DKT.NCHIMBI AAGIZA KUFANYIKA UTAFITI SEKTA YA MISITU

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Emanuel Nchimbi, ameielekeza Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kushirikiana na Taasisi ya utafiti wa Misitu Tanzania (Tafori) kufanya utafiti utakaosaidia kutatua matatizo mbalimbali yanayowakabili Wakulima wa Miti, hususan katika mMsitu ya asili.

Dkt. Nchimbi ametoa maelekezo hayo wakati wa ufunguzi wa Maadhimisho ya Siku ya Misitu Duniani pamoja na Kampeni ya Kitaifa ya Upandaji Miti iliyofanyika katika Manispaa ya Lindi, Mkoani Lindi.

RAIS SAMIA APOKEA RIPOTI YA MABORESHO YA MFUMO WA KODI

Rais Samia Suluhu Hassan amepokea Ripoti ya Tume ya Rais ya kutathmini maboresho ya mfumo wa Kodi Nchini huku akiagiza kuwepo kwa kodi ya haki na usawa kwa Wananchi pamoja na kuwa na tafsiri moja ya sheria ya kodi kati ya Mfanyabiashara na Afisa wa Kodi.

Tume hiyo iliundwa na Rais Dkt.Samia Julai 2024 ili kufanya tathimini ya kina ya Mfumo wa Kodi, kufuatia malalamiko ya muda mrefu kutoka kwa Wawekezaji, na Wafanyabiashara kuhusu changamoto ya mifumo ya kodi Nchini.

BANDARI YA MPIGADURI YAFANYA MAJARIBIO KUSHUSHA MIZIGO

Waziri Wa Ujenzi Na Uchukuzi Zanzibar, Dkt. Khalid Salum Mohamed, Amezindua Majaribio Ya Ushushaji Wa Mizigo Katika Bandari Ya Mpigaduri, Zoezi Lililofanywa Na Meli Za Kampuni Ya Azam Marine.

Akizungumza Wakati Wa Uzinduzi Huo Uliofanyika Waziri Wa Ujenzi Na Uchukuzi Ameeleza Kuridhishwa Na Majaribio Hayo, Huku Akisema Ni Sehemu Ya Jitihada Za Serikali Ya Mapinduzi Ya Zanzibar Kupunguza Msongamano Katika Bandari Ya Malindi.

Amesema Kazi Rasmi La Ushushaji Mizigo Inatarajiwa Kuanza Mwezi Aprili Mwaka Huu Baada Ya Kukamilika Kwa Majaribio Ya Awali. 

Subscribe to
 

Simplenews subscription

The subscriber's email address.
Stay informed - subscribe to our newsletter.