VIONGOZI NA WANANCHI WAJITOKEZA KUTOA HESHIMA ZA MWISHO KWA MHESHIMIWA WILLIAM LUKUVI IRINGA

Ibada ya kumuaga aliyekuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na WenyeUlemavu) na Mbunge wa Isimani, Mheshimiwa William Vangimembe Lukuvi, inafanyika katika Kanisa Kuu la Moyo Mtakatifu wa Yesu, Kichangani, Kihesa, Manispaa ya Iringa.

WIZARA YA AFYA YAFUATILIA MATIBABU YA KIJANA ALIEUMIA KWENYE MAKACHU

Kaimu Waziri Wa Afya Zanzibar Na Waziri Wa Nchi Afisi Ya Raisi Ikulu Dkt. Saada Mkuya Salum,Amesema Serikali Kupitia Wizara Ya Afya Itaendelea Kusimamia Matibabu Ya Abdallah Bakari Aliepata Ajali Ya Kupooza Mwili Ili Kuona Anarudi Katika Hali Yake Ya Kawaida.

Akizungumza Wakati Alipomtembelea Kijana Huyo Na Kuangalia Maendeleo Yake Huko Nyumbani Kwao Jang’ombe,Dkt.Saada Amesema Tokea Kutokea Kwa Ajali Hiyo Serikali Imekuwa Ikichukua Hatua Stahiki Ili Kuona Matibabu Ya Kijana Huyo Yanakwenda Kama Yanavyoelekezwa Na Wataalamu.

Subscribe to
 

Simplenews subscription

The subscriber's email address.
Stay informed - subscribe to our newsletter.