DKT.MWINYI AKAMILISHA KUFUTARISHA KATIKA MIKOA

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt, Hussein Ali Mwinyi amejumuika na Waumini wa Dini ya Kiislamu na Wananchi wa Mkoa wa Kusini katika Futari ya pamoja aliyowaandalia .

MHE.AYOUB ASHIRIKI MKUTANO WA USHIRIKIANO TANZANIA NA UGANDA

Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Ayoub Mohammed Mahmoud, ameshiriki katika Mkutano wa Tano wa Tume ya Pamoja ya Ushirikiano (Joint Permanent Commission - JPC) kati ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Jamhuri ya Uganda uliofanyika kwa lengo la kuimarisha ushirikiano wa pande mbili katika sekta mbalimbali za maendeleo.

Katika mkutano huo uliofanyika leo jijini Dar es Salaam, wajumbe wamejadili masuala mbalimbali ikiwemo mashirikiano ya kidiplomasia na kisiasa, masuala ya ulinzi na usalama pamoja na uhamiaji.

MAFURIKO YAATHIRI NYUMBA 32 NA MASHAMBA KILOSA

Nyumba 32 zimeathiriwa na mafuriko huku Nyumba Sita zikibomoka kabisa  pamoja na Mashamba yenye Mazao mbalimbali yakiwemo Mahindi ekari 300 yamesombwa na maji ya mafuriko katika Kijiji cha Mhenda kilichopo Wilaya ya Kilosa Mkoani Morogoro kutokana na Mvua zinazoendelea kunyesha katika maeneo mbalimbali Wilayani humo.

ZANZIBAR YAIBUKA KIDEDEA MASHINDANO YA KUHIFADHI QUR-AN

Pamoja na Mvua kubwa iliyonyesha katika Visiwa vya Unguja leo, Mashindano makubwa ya Kimataifa ya Kuhifadhi Qur-an yamefanyika kwa ufanisi katika Uwanja wa Amani Complex.

Subscribe to
 

Simplenews subscription

The subscriber's email address.
Stay informed - subscribe to our newsletter.