MHE.AYOUB AWASILISHA BAJETI YA MAMBO YA NDANI 2026 /2027

Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Ayoub Mohammed Mahmoud, amewasilisha Taarifa ya Randama ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Bajeti ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kwa mwaka wa fedha 2026/2027 mbele ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama (NUU)

WASIRA AWEKA JIWE LA MSINGI JENGO LA CCM GEITA

Makamu Mwenyekiti wa CCM (Bara), Stephen Wasira, amewatahadharisha wanachama wa chama hicho kuacha tabia ya kuanzisha mivutano na uchochezi wanapokosa fursa za uteuzi au kushindwa katika kura za maoni.

Akizungumza mkoani Geita wakati wa uwekaji wa Jiwe la msingi la Jengo la Ofisi za Mkoa, Wasira amesisitiza kuwa kukosa uongozi kusitumiwe kama kigezo cha kuvuruga amani ya Chama na Taifa, kwani kufanya hivyo ni kuhatarisha usalama wa Nchi.

TANESCO LINDI YAONGEZA UWEZO WA KITUO CHA MAHUMBIKA KUKIDHI MAHITAJI YA UMEME

Kutokana na ongezeko la mahitaji ya Umeme katika Mikoa ya Lindi na Mtwara, Shirika la Umeme tanzania (TANESCO) Mkoa wa Lindi limeanzisha mradi wa kuongeza uwezo wa kituo cha kupooza umeme cha maumbika kwa kufunga transfoma yenye uwezo wa zaidi ya megawati 15 kwa gharama ya zaidi ya shilingi milioni 702.

DKT. MWIGULU AWAOMBA WATANZANIA KUENDELEA KUMUOMBEA MHE. LUKUVI

WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba amewaomba Watanzania waendelee kumuombea kwa Mwenyezi Mungu aliyekuwa Waziri Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu, marehemu William Lukuvi aliyefariki jana Machi 25, 2026 katika Hospitali ya Benjamin Mkapa, jijini Dodoma.
Akiongea kwa niaba ya Serikali nyumbani kwa marehemu Area D, jijini Dodoma leo, Alhamisi, Machi 26, 2026, Waziri Mkuu amesema: β€œKwa niaba ya Serikali natoa pole kwa familia, ndugu, jamaa. Jambo hili zito, gumu kulielewa, gumu kulipokea.”

Subscribe to
 

Simplenews subscription

The subscriber's email address.
Stay informed - subscribe to our newsletter.