Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Zanzibar (ZAA) kupitia Uwanja wake wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume (AAKIA) umeendelea kushuhudia ongezeko la idadi ya abiria pamoja na miruko ya ndege, huku hatua madhubuti za kuimarisha usalama wa anga zikiendelea kupewa kipaumbele.
