MALIASILI YAZICHAKAZA ARDHI NA RAS NJOMBE
Timu za Mpira wa Miguu Wanaume na Mpira wa Pete za Wizara ya Maliasili na Utalii zimeibuka na ushindi mnono dhidi ya timu za Ardhi na RAS Njombe katika michuano ya Mei Mosi 2026 inayoendelea Mkoani Njombe.
Katika Mchezo wa Mpira wa Pete Wanawake, Timu ya Maliasi imeibuka na ushindi mnono wa magili 34 -13 dhidi ya majirani yao timu ya Wizara ya Ardhi hali iliyo wajaza furaha washabiki wake waliojitokeza kuishangilia.









