RAFAEL NADAL HATI HATI KUREJEA UWANJANI BAADA YA KUUMIA

Rafael Nadal akiwa Uwanjani kabla ya kuumia kwake

Mchezaji namba moja kwa ubora duniani Novak Djokovic anaamini Rafael Nadal atashiriki michuano ya wazi ya Australian Open mwezi ujao, licha ya kuumia kwake.

Mhispania huyo, 37, mshindi wa Grand Slam mara 22, anatazamiwa kurejea Brisbane wikendi hii kabla ya mshindi wa kwanza wa tenisi mwaka huu.

Mechi yake ya mwisho alipoteza kupoteza kwa Mmarekani Mackenzie McDonald katika raundi ya pili kwenye michuano ya Australian Open mwezi Januari.

Toleo la 2024 la mashindano hayo linaanza tarehe 14 Januari huko Melbourne.

Nadal amesema kuwa 2024 huenda ukawa msimu wake wa mwisho kwenye mcezo huo, baada ya kuhitaji kufanyiwa upasuaji wa jeraha la nyonga na kushuka hadi nafasi ya 670 katika viwango vya ubora duniani.

Alishinda Australian Open mnamo 2009 na 2022 na ni bingwa wa rekodi mara 14 kwenye French Open.

Mchezaji namba mbili duniani Carlos Alcaraz, ambaye alicheza na Djokovic katika mechi ya maonyesho mjini Riyadh, Saudi Arabia siku ya Jumatano, pia anaamini kuwa mtani wake yuko tayari kurejea Uwanjani.

Tags
hot
standard
 
The subscriber's email address.
Stay informed - subscribe to our newsletter.