BULGARIA AIR YAANZA RASMI SAFARI ZAKE ZANZIBAR

Mapokezi ya Shirika la Ndege la Bulgaria Air (Bul Air) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume (AAKIA)  Alhamis ya Tarehe 22 Januari 2026

Ndege Aina ya Airbus a 320 iliwasili Uwanjani hapo Majira ya saa 5:30 Asubuhi ikitokea Jijini Sofia ikiwa na Jumla ya Abiria 180.

Shirika hilo la Ndege sasa limeanza rasmi safari zake na linatarajiwa kuwasili Zanzibar MaraTatu kwa Mwezi.

WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AWEKA JIWE LA MSINGI MRADI WA KUSUKUMA NA KUHIFADHI MAJI MWANZA

Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba, ameweka jiwe la msingi la Mradi wa Ujenzi wa Miundombinu ya Kusukuma na Kuhifadhi Maji katika mkoa wa Mwanza, mradi unaolenga kuboresha usambazaji wa maji safi na salama kwa wananchi.

ZANZIBAR YAJITANGAZA KIUTALII LONDON

 Kwa mara ya kwanza katika historia ya Zanzibar imezindua Matangazo ya Utalii katika Jiji la London Nchini Uingereza kwa kubandika Matangazo yanayosomeka Tembelea Zanzibar kwenye Mabasi maarufu ya Abiria yanayoitwa London Buses.    Hatimaye historia imeandikwa.

 Mabango makubwa yanayochagiza, kushajihisha na kuuvutia Utalii wa Zanzibar yameanza kuonekana Leo kwenye Mabasi ya Abira maarufu kama London Luses Nchini Uingereza.

WANASWA KWA KUHUJUMU MRADI WA MAJI WA MIJI 28

WATU wanne wamekamatwa na Jeshi la Polisi Mkoani Tabora kwa tuhuma za kuhujumu Mradi wa Maji wa Miji 28 unaoendelea kutekelezwa na serikali katika Wilaya za Sikonge, Urambo na Kaliua ili kumaliza kero ya wananchi.

Kaimu Kamanda wa Polisi ACP Constatine Mbogambi amethibitisha kukamatwa watuhumiwa hao wakiwa na vifaa mbalimbali vilivyoibiwa kwenye mradi huo Wilayani Urambo. Akitaja baadhi ya vifaa vilivyokamatwa kuwa ni mashine kubwa 3 za kuchomelea mabomba, grenda mashine 2 za kukatia mabomba, nyaya 9 za kuunganishia grenda hizo na lita 40 za mafuta ya mitambo ya hydroliki.

Subscribe to
 

Simplenews subscription

The subscriber's email address.
Stay informed - subscribe to our newsletter.