WANAOSAFIRISHA MAGENDO WATAKIWA KUCHUKULIWA HATUA

Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Kusini Pemba ambaye pia ni Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Pemba Mgeni Khatib Yahya ameagiza kuchukuliwa hatua kali za kisheria dhidi ya wale waliohusika kutaka kutorosha Magunia 15 ya Karafuu katika Bandari ya Wambaa Wilaya ya Mkoani

MFUMO MPYA WA KUSAMBAZA DAWA ZA KULEVYA WAGUNDULIWA

Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya Zanzibar imewakamata Watuhumiwa Watatu wanaosadikiwa kusambaza na kuuza Dawa za kulevywa kwa kutumia mbinu mpya ambayo ni kuchanganya na Dawa za Binaadamu

Akitoa Taarifa kwa Waandishi wa Habari Ofisini kwake Migombani Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya Zanzibar Kanali Burhani Zubeiri Nassoro amesema bidhaa hizo zenye vifungashio zimekamatwa katika Maduka mabali mbali hapa Zanzibar

WATOTO WENYE ULEMAVU WATOA KILIO CHAO HADHARANI

Wadau wa Maendeleo, Watunga Sera, Mashirika yasiyo ya Kiserikali pamoja na asasi za kiraia kutoka Nchi 23 Duniani wamekutana Jijini Arusha katika Jukwaa la Kimataifa la kujifunza kuhusu usawa wa kijinsia, ujumuishi wa watu wenye ulemavu na ushirikishwaji wao katika Jamii.

Subscribe to
 

Simplenews subscription

The subscriber's email address.
Stay informed - subscribe to our newsletter.