WAFANYABIASHARA SOKO LA KINYASINI WALIA NA MIUNDOMBINU ISIYO RAFIKI

Wafanyabiashara wa Soko la Kinyasini Wilaya ya Kaskazini 'a' Unguja wamesema kuwa Eneo la Soko ni dogo kwa kufanyia biashara zao na linasababisha msongamano baina ya Wafanyabiashra na Wateja.

 Wakizungumza na Kamera ya Biashara na Uchumi ZBC Wafanyabiashara hao wamesema Soko hilo halikidhi kuchukua Watu wengi hali inayopelekea baadhi ya Wafanyabiashara kupanga bidhaa chini na pembezoni mwa barabara. 

HUDUMA ZA KIBINGWA 20 ZATOLEWA HOSPITALI YA BENJAMIN MKAPA

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt.Hussein Ali Mwinyi ameipongeza Hospitali ya Benjamin Mkapa kwa mageuzi namafanikio makubwa ya utoaji wa huduma za matibabu ya kibingwa kwa Wananchi. 

Akizungumza na Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali hiyo Prof. Abel Makubi akiambatana na ujumbe wake waliofika Ikulu Zanzibar Dķt.Mwinyi amesifia huduma hizo ikiwemo matibabu ya Figo ,Moyo na Ubongo kufanyika hapa Nchini ,hatua aliyopunguzia Serikali na Wananchi gharama za kuwapeleka Wagonjwa Nje ya Nchi.

Subscribe to
 

Simplenews subscription

The subscriber's email address.
Stay informed - subscribe to our newsletter.