DKT. MWINYI AFUNGUA VIWANJA VYA MATUMBAKU SPORTS COMPLEX

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amesema Serikali itaendelea kujenga  miundombinu ya  viwanja vya michezo ili kuwawezesha vijana kujiajiri kupitia michezo.

Akifungua viwanja vipya vya Matumbaku Sports Complex vinavyo jumuisha michezo mbali mbali ikiwemo mpira wa wavu ,kikapu, mpira wa Pete na mpira miguu, Dkt. Mwinyi amesema Kutokana na ukuaji wa soko la Ajira Duniani kupitia michezo, Serikali imeona ipo haja ya kuimarishwa viwanja hivyo ili kukuza utalii na kuimarisha uchumi wa nchi.

CARLO ANCELOTTI BADO YUPO SANA REAL MADRID HADI 2026

Meneja wa Real Madrid, Carlo Ancelotti ametia saini mkataba mpya na klabu hiyo utakaodumu hadi Juni 2026.

Muitaliano huyo, mwenye umri wa miaka 64, aliteuliwa Bernabeu kwa mara ya pili mwaka 2021 kwa mkataba wa awali wa miaka mitatu.

 

Alihusishwa na kuchukua nafasi ya meneja wa Brazil mapema mwaka huu lakini akasema anataka kubaki katika klabu hiyo.

 

Ancelotti ameshinda mataji 10 kama kocha wa Real, yakiwemo mawili ya Ligi ya Mabingwa - hivi karibuni katika msimu wake wa kwanza akiwa na klabu hiyo mnamo 2021-22.

 

EMMA KUREJEA TENA KUCHEZA TENNIS BAADA YA UPASUAJI WA MIKONO

Mwingereza Emma Raducanu anasema anahisi kuzaliwa upya wakati huu, akijiandaa kurejea tena kwenye tenisi huko Auckland baada ya miezi minane nje ya uwanja.

Bingwa wa US Open 2021 alicheza mechi tisa pekee mnamo 2023, akiwa nje ya uwanja tangu Aprili.

Raducanu, mwenye umri wa miaka 21, alifanyiwa upasuaji wa mikono yote miwili na kifundo cha mguu wake wa kushoto mwezi Mei, na ameshuka hadi nafasi ya 298 katika viwango vya ubora duniani.

AKRAM NI NYOTA WA KWANZA KUFUNGA BAO UWANJA WA NEW AMAAN COMPLEX.

Nyota wa klabu ya KVZ, Akram Mhina Omar ndie mchezaji wa kwanza kufunga bao katika Uwanja wa New Amaan Complex, baada ya matengenezo makubwa yaliyochukua takribani miezi Sita, katika mchezo wa michuano ya Mapinduzi Cup dhidi ya Jamhuri.

New Amaan Compex, ulifunguliwa rasmi Disemba 27, 2023 saa kumi na moja dakika 23 jioni, na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Ali Mwinyi baada ya ukarabati huo kupita.

Subscribe to
 

Simplenews subscription

The subscriber's email address.
Stay informed - subscribe to our newsletter.