Meneja wa Real Madrid, Carlo Ancelotti ametia saini mkataba mpya na klabu hiyo utakaodumu hadi Juni 2026.
Muitaliano huyo, mwenye umri wa miaka 64, aliteuliwa Bernabeu kwa mara ya pili mwaka 2021 kwa mkataba wa awali wa miaka mitatu.
Alihusishwa na kuchukua nafasi ya meneja wa Brazil mapema mwaka huu lakini akasema anataka kubaki katika klabu hiyo.
Ancelotti ameshinda mataji 10 kama kocha wa Real, yakiwemo mawili ya Ligi ya Mabingwa - hivi karibuni katika msimu wake wa kwanza akiwa na klabu hiyo mnamo 2021-22.