Mwekezaji wa klabu ya Simba na Mfanyabiashara Mohammed Dewij ameibuka Mtandao na kuhoji hatua iliyofikiwa katika mchakato wa Mabadiliko ya Mfumo wa uendeshaji wa Klabu ya Simba.
Swali hilo limeibuka wakati Uongozi wa klabu ukitangaza rasmi kurejesha usajili wa wanachama kwenye mkutano wake na Vyombo vya Habari Jijini Dar es Salaam. Leo Februari 10,2026.

Mo, Dewij amehoji kupitia Taarifa aliyonukuliwa Mwenyekiti wa Klabu ya Simba SC, Murtaza Mangungu kupitia ukurasa rasmi wa Simba wakati wa Mkutano “Transformation mmefikia wapi ”.? Alihoji Mwekezaji wa Klabu Mo Dewiji
Swali hilo limeendelea kuchukua sura Mpya huku baadhi ya Mashabiki na Wadau wa soka wakiuliza inakuwaje
Mwekezaji aulize swali la kiutawala Mtandaoni huku wengine wakihoji ushiriki wake ndani ya Klabu ya Simba.
Mtazamo wako ni upo juu ya Mjadala huu ambao unaendelea kuibua hisia mpya ndani ya klabu .?
