FUKWE YA FORODHANI SI SALAMA KWA WATOTO KUOGELEA

Kumekuwa na Ongezeko la matukio ya ajali za kuzama kwa Watoto na hata Watu Wazima mara kwa mara katika Eneo la Forodhani. Eneo hilo linatajwa kuwa na kina kirefu cha Maji na hakuna maelekezo ya Tahadhari.

Hapana shaka kwamba Eneo la Forodhani hapa Zanzibar ni moja ya Maeneo yenye Fukwe safi na haiba si tu kustarehe, lakini ile sura ya Utalii wa Zanzibar. hata hivyo baadhi ya Maeneo ya Fukwe hiii maarufu kwa sasa ni hatarishi hususani kwa Watoto kuogelea ama Mtu asiye na ujuzi wa Kuogelea.

DKT.SAMIA AWATAKA WATANZANIA KUJENGA UTAMADUNI WA KULINDA MAZINGIRA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan Ametoa wito kwa Watanzania kuendelea kujenga utamaduni wa kulinda na kuhifadhi mazingira kwa hiari wakitambua kuwa ulinzi wa mazingira ni msingi wa uhai, maendeleo na usalama wa Taifa.

Rais Samia ameongoza mchakato wa upandaji miti katika Maeneo ya Bungi kilimo pamoja na Kizimkazi ikiwa ni kuadhimisha Siku yake ya Kuzaliwa ambapo amesisitiza Watanzania kuimarisha uoto wa asili na kuchangia kwa vitendo juhudi za kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabia Nchi kwa ustawi wa Maendeleo ya Taifa.

SERIKALI YASAINI MKATABA UJENZI HOSPITALI YA MKOA MAHONDA

 Wizara ya Afya Zanzibar imetiliana Saini Mkataba wa Ujenzi wa Hospital ya Mkoa Mahonda na Kampuni Cross World Construction Limited.

Akizungumza baada ya Utaji Saini Mkataba huo Kaimu Waziri wa Afya Zanzibar Dkt. Saada Mkuya Salum amesema Mradi huo utakua ufumbuzi wa upatikanaji wa huduma za Kibingwa za Afya na kuipunguzia gharama Serikali ya kusafirisha Wagonjwa kutoka Nje ya Nchi.

HISTORIA YAANDIKWA MABASI YA UMEME YAWASILI ZANZIBAR

Zanzibar imeandika historia Barani Afrika baada ya kuingiza Mabasi ya Umeme kwa mara ya kwanza. Serikali kupitia mradi wa usafiri wa kisasa imepokea Mabasi Kumi ya Umeme, ikiwa ni hatua ya Mwanzo ya mpango wa kuingiza Jumla ya Mabasi Mia Moja. 

Mabasi hayo yanatarajiwa kuanza kufanya kazi rasmi Mwezi wa Tatu baada ya kukamilika kwa taratibu na Sheria husika. hatua hii inalenga kuboresha Usafiri wa Umma na kupunguza uchafuzi wa Mazingira.

BULGARIA AIR YAANZA RASMI SAFARI ZAKE ZANZIBAR

Mapokezi ya Shirika la Ndege la Bulgaria Air (Bul Air) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume (AAKIA)  Alhamis ya Tarehe 22 Januari 2026

Ndege Aina ya Airbus a 320 iliwasili Uwanjani hapo Majira ya saa 5:30 Asubuhi ikitokea Jijini Sofia ikiwa na Jumla ya Abiria 180.

Shirika hilo la Ndege sasa limeanza rasmi safari zake na linatarajiwa kuwasili Zanzibar MaraTatu kwa Mwezi.

ZANZIBAR YAJITANGAZA KIUTALII LONDON

 Kwa mara ya kwanza katika historia ya Zanzibar imezindua Matangazo ya Utalii katika Jiji la London Nchini Uingereza kwa kubandika Matangazo yanayosomeka Tembelea Zanzibar kwenye Mabasi maarufu ya Abiria yanayoitwa London Buses.    Hatimaye historia imeandikwa.

 Mabango makubwa yanayochagiza, kushajihisha na kuuvutia Utalii wa Zanzibar yameanza kuonekana Leo kwenye Mabasi ya Abira maarufu kama London Luses Nchini Uingereza.

Subscribe to ZBC
 

Simplenews subscription

The subscriber's email address.
Stay informed - subscribe to our newsletter.