WAZIRI MKUU ATAKA JUHUDI ZA UPATIKANAJI MAJI ZIONGEZWE
Waziri Mkuu Wa Tanzania Dkt. Mwigulu Nchemba Amezindua Teknolojia Mpya Ya Ulipaji Wa Bili Za Maji Kwa Njia Ya Mtandao Na Kuwataka Wakurugenzi Wa Mamlaka Za Maji Safi Na Usafi Wa Mazingira Nchini Kuongeza Juhudi Katika Maeneo Ambayo Bado Wananchi Wanakabiliwa Na Changamoto Ya Upatikanaji Wa Maji.
Dkt. Nchemba Ameyasema Hayo Wakati Akifungua Mkutano Wa Bodi Za Wakurugenzi Wa Mamlaka Za Maji Safi Na Usafi Wa Mazingira Nchini, Mkutano Ulio Lenga Kuwanoa Watendaji Wa Sekta Hiyo Ili Kuongeza Ufanisi Na Uwajibikaji Katika Utekelezaji Wa Miradi Ya Maji.


