WAZIRI MKUU ATAKA JUHUDI ZA UPATIKANAJI MAJI ZIONGEZWE

Waziri Mkuu Wa Tanzania Dkt. Mwigulu Nchemba Amezindua Teknolojia Mpya Ya Ulipaji Wa Bili Za Maji Kwa Njia Ya Mtandao Na Kuwataka Wakurugenzi Wa Mamlaka Za Maji Safi Na Usafi Wa Mazingira Nchini Kuongeza Juhudi Katika Maeneo Ambayo Bado Wananchi Wanakabiliwa Na Changamoto Ya Upatikanaji Wa Maji.

Dkt. Nchemba Ameyasema Hayo Wakati Akifungua Mkutano Wa Bodi Za Wakurugenzi Wa Mamlaka Za Maji Safi Na Usafi Wa Mazingira Nchini, Mkutano Ulio Lenga Kuwanoa Watendaji Wa Sekta Hiyo Ili Kuongeza Ufanisi Na Uwajibikaji Katika Utekelezaji Wa Miradi Ya Maji.

DKT.MWIGULU ATOA WIKI MBILI KWA WIZARA YA MAJI KUTAFUTA MKANDARASI

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Mwigulu Nchemba ameipa Wizara ya Maji Wiki mbili kuhakikisha inakamilisha utaratibu wa upatikanaji wa Mkandarasi wa Ujenzi wa Mradi wa Maji kutoka chanzo cha Ziwa Chala.

Ametoa agizo hilo wakati akizungumza na Wananchi wa Kata ya Marangu-Kitowo, Wilaya ya Rombo Mkoani Kilimanjaro baada ya kupokea taarifa za Ujenzi wa Mradi wa Maji kutoka chanzo cha Ziwa Chala, Ujenzi wa Mradi wa Barabara holili(Rotima)-tarakea(nayemi), pamoja kuweka jiwe la msingi la skuli ya sekondari stephen moshi technical. 

UWEKEZAJI ZANA ZA KILIMO AFRIKA HAIENDANI NA MAHITAJI HALISI

Tanzania Kwa Kushirikiana Na Shirika La Kilimo Na Chakula La Umoja Wa Mataifa (Fao) Imeandaa Mkakati Wa Taifa Wa Zana Za Kilimo Unaolenga Kuimarisha Matumizi Ya Uzalishaji, Usimamizi Na Uratibu Wa Teknolojia Za Kilimo.

Subscribe to WAZIRI MKUU TANZANIA
 

Simplenews subscription

The subscriber's email address.
Stay informed - subscribe to our newsletter.