WATOTO WENYE ULEMAVU WATOA KILIO CHAO HADHARANI

Wadau wa Maendeleo, Watunga Sera, Mashirika yasiyo ya Kiserikali pamoja na asasi za kiraia kutoka Nchi 23 Duniani wamekutana Jijini Arusha katika Jukwaa la Kimataifa la kujifunza kuhusu usawa wa kijinsia, ujumuishi wa watu wenye ulemavu na ushirikishwaji wao katika Jamii.

SERIKALI KUMALIZA MIGOGORO YA ARDHI IFIKAPO 2030

Waziri wa Ardhi na Maendeleo ya Makaazi Mhe. Rahma Kassim Ali ameeleza azma ya Serikali ni kumaliza migogoro ya ardhi ifikapo 2030 kupitia Mradi wa Mfumo wa Usimamizi na Usajili wa Ardhi (laris).

DKT. MWIGULU AAGIZA KUCHUKULIWA HATUA MKANDARASI MANYARA

Waziri Mkuu wa Tanzania Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba, amemuagiza Mkuu wa Mkoa wa Manyara, kumchukulia hatua Mkandarasi wa mradi wa kuboresha miundombinu ya Miji Tanzania (Tactics).

Agizo hilo amelitoa kufuatia kucheleweshwa kwa mradi huo wenye thamani ya Shilingi Bilioni 19.9, unaojumuisha Ujenzi wa Bararaba, Mitaro pamoja na Ujenzi wa Stendi ya Mkoa wa Manyara ambapo mpaka sasa Ujenzi wa stendi hiyo umefikia asilimia 10 tu.

SERIKALI KUTUMIA BILIONI 79 KUJENGA VITUO VYA POLISI 698 NCHI NZIMA

Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Ayoub Mohammed Mahmoud, amesema Serikali imepanga kutumia zaidi ya Shilingi Bilioni 79 kwa ajili ya ujenzi wa vituo vya polisi 698 nchini, ikiwa ni mkakati wa kuimarisha usalama wa raia na mali zao.

​Akizungumza leo wakati wa ziara yake ya kukagua miradi ya Vituo vya Jeshi la Polisi visiwani Zanzibar Mhe. Ayoub Mahmoud amebainisha kuwa uamuzi huo umekuja baada ya Serikali kuona kuna uhitaji wa kusogeza huduma za Kipolisi karibu na wananchi zaidi.

KIKOSI CHA ZIMAMOTO CHAPOKEA GARI TISA NA BOTI 1

Kamishna wa Kikosi cha Zimamoto na Uokozi Zanzibar Rashid Mzee Abdallah amesema Kikosi hicho kinaendelea kujiimarisha kwa kuwa na Vifaa vya kisasa vya kukabiliana na Majanga ya Moto.

 

Kamishna Rashid ameyasema hayo baada ya kupokea Gari Tisa za Kuzimia Moto na Boti moja kutoka Nchini Austria.

BILIONI MIA SABA ZATUMIKA KUJENGA KIWANDA CHA SUKARI KILOMBERO

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais mipango na uwekezaji Professa Kitila Mkumbo amesema kiwanda kipya cha sukari Kilombero K4  kilichopo Mkoani Morogoro ambacho kinajengwa kwa gharama ya shilingi Billioni mia saba kinatarajiwa kuanza uzalishaji wake Mwezi Juni Mwaka huu ni moja ya Kiwanda ambacho kitafanya lengo ya kukuza uchumi kuelekea Mwaka 2050  kufikia dola trilioni moja.

DKT. MKUYA ATAKA WACHUKULIWE HATUA WAHUDUMU WASIOWASIJIBIKA

Kaimu Waziri Wa Afya Zanzibar Na Waziri Wa Nchi Afisi Ya Raisi Ikulu Dkt Saada Mkuya Salum Amewataka Madaktari Dhamana Ngazi Ya Wilaya Kufanya Kazi Kwa Weledi Ili Sekta Ya Afya Ieandane Na Uwekezaji Uliofanywa Na Serikali.

Akizungumza Katika Mkutano Maalumu Na Viongozi Wa Wizara Ya Afya Pamoja Na Madaktari Hao Dkt. Saada Amesema Kwa Sasa Wananchi Wamekuwa Wakilalamikia Juu Ya Huduma Wanazozipata Katika Vituo Vya Afya Pamoja Na Hospitali, Jambo Ambalo Limekuwa Likiongeza Matatizo Kwa Wagonjwa Wanaofuata Huduma Katika Hospitali Hizo.

WAZIRI MKUU ATAKA JUHUDI ZA UPATIKANAJI MAJI ZIONGEZWE

Waziri Mkuu Wa Tanzania Dkt. Mwigulu Nchemba Amezindua Teknolojia Mpya Ya Ulipaji Wa Bili Za Maji Kwa Njia Ya Mtandao Na Kuwataka Wakurugenzi Wa Mamlaka Za Maji Safi Na Usafi Wa Mazingira Nchini Kuongeza Juhudi Katika Maeneo Ambayo Bado Wananchi Wanakabiliwa Na Changamoto Ya Upatikanaji Wa Maji.

Dkt. Nchemba Ameyasema Hayo Wakati Akifungua Mkutano Wa Bodi Za Wakurugenzi Wa Mamlaka Za Maji Safi Na Usafi Wa Mazingira Nchini, Mkutano Ulio Lenga Kuwanoa Watendaji Wa Sekta Hiyo Ili Kuongeza Ufanisi Na Uwajibikaji Katika Utekelezaji Wa Miradi Ya Maji.

MAPIPA 88 YA DIZEL YAKAMATWA YAKISAFIRISHWA KIMAGENDO

Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Pemba, Mgeni Khatib Yahya, amewatahadharisha Wananchi wanaotumia Bandari Bubu  kufanya magendo kuacha vitendo hivyo, kwani Serikali haitasita kuchukua hatua kali za kisheria dhidi yao.

DKT. MWINYI AHIMIZA VIJANA KUSOMA QUR-AN ILI KUJENGA KIZAZI CHENYE MAADILI

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amesisitiza umuhimu wa kuendeleza utaratibu wa kuisoma, kuihifadhi na kuzingatia mafundisho ya Qur-ani Tukufu miongoni mwa Vijana ili kujenga kizazi chenye Maadili, hofu ya Mwenyezi Mungu na mchango mzuri katika Jamii.

Subscribe to news
 

Simplenews subscription

The subscriber's email address.
Stay informed - subscribe to our newsletter.