DKT. MWINYI ASHIRIKI MAZISHI YA MAMA WA KAMANDA DAIMA
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Hussein Ali Mwinyi amejumuika na Viongozi mbalimbali wa Serikali katika Maziko ya Bibi Sichana Is-haka Daima Mama Mzazi wa Kamanda Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKU) Kanali Makame Abdalla Daima.
Marehemu Sichana Daima Amefariki Jana wakati akitibiwa katika Hospitali ya Mkoa Lumumba. Awali Dkt. Mwinyi alishiriki Sala ya Maiti katika Msikiti wa Bumbwini Misufini.









