DKT.NCHIMBI AAGIZA KUFANYIKA UTAFITI SEKTA YA MISITU
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Emanuel Nchimbi, ameielekeza Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kushirikiana na Taasisi ya utafiti wa Misitu Tanzania (Tafori) kufanya utafiti utakaosaidia kutatua matatizo mbalimbali yanayowakabili Wakulima wa Miti, hususan katika mMsitu ya asili.
Dkt. Nchimbi ametoa maelekezo hayo wakati wa ufunguzi wa Maadhimisho ya Siku ya Misitu Duniani pamoja na Kampeni ya Kitaifa ya Upandaji Miti iliyofanyika katika Manispaa ya Lindi, Mkoani Lindi.










