DKT.NCHIMBI AAGIZA KUFANYIKA UTAFITI SEKTA YA MISITU

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Emanuel Nchimbi, ameielekeza Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kushirikiana na Taasisi ya utafiti wa Misitu Tanzania (Tafori) kufanya utafiti utakaosaidia kutatua matatizo mbalimbali yanayowakabili Wakulima wa Miti, hususan katika mMsitu ya asili.

Dkt. Nchimbi ametoa maelekezo hayo wakati wa ufunguzi wa Maadhimisho ya Siku ya Misitu Duniani pamoja na Kampeni ya Kitaifa ya Upandaji Miti iliyofanyika katika Manispaa ya Lindi, Mkoani Lindi.

RAIS SAMIA APOKEA RIPOTI YA MABORESHO YA MFUMO WA KODI

Rais Samia Suluhu Hassan amepokea Ripoti ya Tume ya Rais ya kutathmini maboresho ya mfumo wa Kodi Nchini huku akiagiza kuwepo kwa kodi ya haki na usawa kwa Wananchi pamoja na kuwa na tafsiri moja ya sheria ya kodi kati ya Mfanyabiashara na Afisa wa Kodi.

Tume hiyo iliundwa na Rais Dkt.Samia Julai 2024 ili kufanya tathimini ya kina ya Mfumo wa Kodi, kufuatia malalamiko ya muda mrefu kutoka kwa Wawekezaji, na Wafanyabiashara kuhusu changamoto ya mifumo ya kodi Nchini.

BANDARI YA MPIGADURI YAFANYA MAJARIBIO KUSHUSHA MIZIGO

Waziri Wa Ujenzi Na Uchukuzi Zanzibar, Dkt. Khalid Salum Mohamed, Amezindua Majaribio Ya Ushushaji Wa Mizigo Katika Bandari Ya Mpigaduri, Zoezi Lililofanywa Na Meli Za Kampuni Ya Azam Marine.

Akizungumza Wakati Wa Uzinduzi Huo Uliofanyika Waziri Wa Ujenzi Na Uchukuzi Ameeleza Kuridhishwa Na Majaribio Hayo, Huku Akisema Ni Sehemu Ya Jitihada Za Serikali Ya Mapinduzi Ya Zanzibar Kupunguza Msongamano Katika Bandari Ya Malindi.

Amesema Kazi Rasmi La Ushushaji Mizigo Inatarajiwa Kuanza Mwezi Aprili Mwaka Huu Baada Ya Kukamilika Kwa Majaribio Ya Awali. 

DKT.MWINYI AKAMILISHA KUFUTARISHA KATIKA MIKOA

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt, Hussein Ali Mwinyi amejumuika na Waumini wa Dini ya Kiislamu na Wananchi wa Mkoa wa Kusini katika Futari ya pamoja aliyowaandalia .

MHE.AYOUB ASHIRIKI MKUTANO WA USHIRIKIANO TANZANIA NA UGANDA

Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Ayoub Mohammed Mahmoud, ameshiriki katika Mkutano wa Tano wa Tume ya Pamoja ya Ushirikiano (Joint Permanent Commission - JPC) kati ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Jamhuri ya Uganda uliofanyika kwa lengo la kuimarisha ushirikiano wa pande mbili katika sekta mbalimbali za maendeleo.

Katika mkutano huo uliofanyika leo jijini Dar es Salaam, wajumbe wamejadili masuala mbalimbali ikiwemo mashirikiano ya kidiplomasia na kisiasa, masuala ya ulinzi na usalama pamoja na uhamiaji.

MAFURIKO YAATHIRI NYUMBA 32 NA MASHAMBA KILOSA

Nyumba 32 zimeathiriwa na mafuriko huku Nyumba Sita zikibomoka kabisa  pamoja na Mashamba yenye Mazao mbalimbali yakiwemo Mahindi ekari 300 yamesombwa na maji ya mafuriko katika Kijiji cha Mhenda kilichopo Wilaya ya Kilosa Mkoani Morogoro kutokana na Mvua zinazoendelea kunyesha katika maeneo mbalimbali Wilayani humo.

ZANZIBAR YAIBUKA KIDEDEA MASHINDANO YA KUHIFADHI QUR-AN

Pamoja na Mvua kubwa iliyonyesha katika Visiwa vya Unguja leo, Mashindano makubwa ya Kimataifa ya Kuhifadhi Qur-an yamefanyika kwa ufanisi katika Uwanja wa Amani Complex.

SEKTA YA AFYA ZANZIBAR NI YA KUPIGIWA MFANO

Lusi Nikolaieva Raia wa Ukraine ameisifu Sekta ya Afya Zanzibar kwa kuwekeza katika huduma ya Mama na Mtoto iliyomsaidia kujifungua salama hapa Zanzibar tofauti na mategemeo yake 

Amesema Wanawake wa ndani na nje hawana haja ya kuwa na wasiwasi kwani uwekezaji wa Zanzibar katika Hospital za Serikali ni sawa na Hospital binafsi Bara la Ulaya 

Moja ya Watu aliowataja Lusi katika safari yake ya kupata huduma bora ni Muuguzi Maryam na hapa anatueleza hatua hiyo ilivyompa uzoefu na kuongeza maarifa kwa kujisikia fahari katika kazi yake 

RAIS SAMIA AMEMUASILI MTOTO ALIYETELEKEZWA TABORA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan amemuasili Mtoto mchanga wa kike aliyekuwa ametupwa na kutelekezwa huko Wilayani Nzega Mkoani Tabora.

Shughuli ya kumuasili Mtoto huyo imefanyika leo Ikulu ya Chamwino Mkoani Dodoma.

WANAWAKE WAHIMIZWA KUSIMAMIA MALEZI

Baada ya kufanikiwa kiuchumi Wanawake Nchini wameaswa kuzingatia mila na desturi zinazojenga na sio kubomoa na kuharibu kizazi cha baadae

Kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani Mkoani Geita kilopambwa na ujumbe mzito wa kuwataka Wanawake Nchini kuoanisha mafanikio ya kiuchumi na utunzaji wa mila na desturi bora.

Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi maalum, Dkt. Dorothy Gwajima, amesisitiza kuwa juhudi za Serikali za kumuinua Mwanamke kiuchumi hazina lengo la kubomoa misingi ya Familia, bali ni kupunguza ukatili Majumbani.

Subscribe to news
 

Simplenews subscription

The subscriber's email address.
Stay informed - subscribe to our newsletter.