MKUU WA MKOA WA PWANI, RC KUNENGE ASHIRIKI ZOEZI LA KUPANDA MITI

Katika kusheherekea sikukuu ya kuzaliwa kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan, Mkuu wa Mkoa wa Pwani Alhaji Abubakari  Kunenge ameshiriki zoezi la upandaji wa miti katika shule ya Msingi Chumbi 'A' Wilayani Rufiji Mkoani Pwani.

DKT.SAMIA AWATAKA WATANZANIA KUJENGA UTAMADUNI WA KULINDA MAZINGIRA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan Ametoa wito kwa Watanzania kuendelea kujenga utamaduni wa kulinda na kuhifadhi mazingira kwa hiari wakitambua kuwa ulinzi wa mazingira ni msingi wa uhai, maendeleo na usalama wa Taifa.

Rais Samia ameongoza mchakato wa upandaji miti katika Maeneo ya Bungi kilimo pamoja na Kizimkazi ikiwa ni kuadhimisha Siku yake ya Kuzaliwa ambapo amesisitiza Watanzania kuimarisha uoto wa asili na kuchangia kwa vitendo juhudi za kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabia Nchi kwa ustawi wa Maendeleo ya Taifa.

AJALI YA BASI NA LORI YAUA MMOJA NA KUJERUHI 12 SHINYANGA

Basi la Kampuni ya Kisire limegongana uso kwa uso na lori katika eneo la mnada wa Tinde Wilaya ya Shinyanga na kusababisha kifo cha mtu mmoja huku wengine 12 wakijeruhiwa na kukimbizwa Kituo cha afya Tinde kupata matibabu.

Ajali hiyo imehusisha basi la Kisire lenye namba za usajili T 229 EEL, lililokuwa likitoka Kahama kuelekea Mwanza, kugongana uso kwa uso na lori la mizigo lenye namba za usajili RAE 849N. lililokuwa limebeba shehena ya mchele kutoka Dar es Salaam kwenda nchi jirani ya Rwanda huku chanzo kikielezwa kuwa ni mwendo kasi.

MWENYEKITI RAJABU, TANGA NDIO CHIMBUKO LA SOKA NCHINI

Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Tanga Rajabu Abdallah amesema mkoa huo ndio chimbuko la vilabu vya mpira nchini,hivyo wadau waunge mkono timu za eneo hilo ili kufufua ushindani uliokuwepo.

Akizungumza  wakati wa sherehe za kukabidhi basi kwaajili ya timu ya mpira wa miguu ya African Sports Club zilizofanyika makao makuu ya timu hiyo mwenyekiti Rajabu amesema timu hiyo na Coastal Union ushabiki wake ni zaidia ya Simba na Yanga.

RC TANGA ATOA AGIZO KWA WAKUU WA WILAYA KUHUSU WAMACHINGA

Mkuu wa mkoa wa Tanga Balozi Batilda Buriani amewaagiza wakuu wa wilaya zote za eneo hilo kuwatafutia maeneo ya uhakika wafanyabiashara ndogondogo maarufu kama Machinga,na katafuta sehemu ambayo watakaa bila changamoto

Akizungumza wakati akifunga maadhimisho ya wiki ya huduma za fedha kitaifa yaliofanyika mkoani Tanga katika viwanja vya shule ya sekondari usagara kwa wiki moja Jumatatu Januari 26,2026 Balozi Batilda amesema wafanyabiashara ndogondogo wanatakiwa kuwekwa sehemu  nzuri.

HATUJAANGUSHA NDEGE NI ZOEZI LA UTAYARI (ZAA)

Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Zanzibar (ZAA) imefanya zoezi la utayari ikiwa ni sehemu ya majukumu yake ya kawaida ya usalama wa anga katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume (AAKIA), lenye lengo la kupima uwezo wa kukabiliana na matukio ya dharura yanayoweza kutokea katika Viwanja vya Ndege.

NGUVU YA PAMOJA INAHITAJIKA KUKOMESHA UKATILI WA KIJINSIA

Nairat Abdallah Ali ndie Mkurugenzi mpya wa Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake TAMWA Zanzibar 

Nairat anachukuwa nafasi hiyo kutoka kwa Dkt. Mzuri Issa aliyehudumu katika nafasi hiyo kwa Kipindi cha Miaka 19

 

 

ZANZIBAR YAJIANDAA NA DHARURA ZA NDEGE

Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Zanzibar imefanikiwa kutekeleza zoezi la kujiandaa na kukabiliana na dharura za Ndege, hatua inayolenga kuimarisha uratibu kati ya Taasisi za Ulinzi, usalama na usimamizi wa maafa.  Zoezi hilo limefanyika katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa Abeid Amani Karume 

Hayo yamebainishwa na Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Zanzibar Mulhat Yussuf Said wakati akizungumza na Waandishi wa Haaabari 

TUME YA TAIFA YA MIPANGO YA MATUMIZI YA ARDHI YATATUA MGOGORO ULIODUMU MIAKA 10 WILAYA YA KISARAWE

Tume ya Taifa ya Mipango ya Matumizi ya Ardhi (NLUPC) imefanikiwa kutatua mgogoro  wa mpaka  kati ya vijiji viwili uliyodumu zaidi ya  miaka kumi huko Wilaya Kisarawe Mkoani Pwani.

SERIKALI YASAINI MKATABA UJENZI HOSPITALI YA MKOA MAHONDA

 Wizara ya Afya Zanzibar imetiliana Saini Mkataba wa Ujenzi wa Hospital ya Mkoa Mahonda na Kampuni Cross World Construction Limited.

Akizungumza baada ya Utaji Saini Mkataba huo Kaimu Waziri wa Afya Zanzibar Dkt. Saada Mkuya Salum amesema Mradi huo utakua ufumbuzi wa upatikanaji wa huduma za Kibingwa za Afya na kuipunguzia gharama Serikali ya kusafirisha Wagonjwa kutoka Nje ya Nchi.

Subscribe to news
 

Simplenews subscription

The subscriber's email address.
Stay informed - subscribe to our newsletter.