WIZARA YA NISHATI IMEKABIDHI VITENDEA KAZI KWA TANESCO KUIMARISHA HUDUMA

Wizara ya Nishati imechukuwa  hatua mpya ya kuimarisha huduma za umeme Mkoani Shinyanga  baada ya Shirika la Umeme Tanzania  TANESCO kupatiwa vitendea kazi vitakavyorahisisha kuwafikia wananchi wengi zaidi, hususan waishio vijijini na maeneo ya pembezoni.

WASIRA AWEKA JIWE LA MSINGI JENGO LA CCM GEITA

Makamu Mwenyekiti wa CCM (Bara), Stephen Wasira, amewatahadharisha wanachama wa chama hicho kuacha tabia ya kuanzisha mivutano na uchochezi wanapokosa fursa za uteuzi au kushindwa katika kura za maoni.


 

MAFUNZO YA COPRA YAWANOA MAAFISA UGANI 75 MOROGORO

Mamlaka ya Udhibiti wa Nafaka na Mazao Mchanganyiko (COPRA) imeendesha mafunzo maalum kwa Maafisa Ugani kata 75 wa Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro, ikiwa ni sehemu ya juhudi za Serikali kuimarisha sekta ya kilimo kama mhimili mkuu wa uchumi wa wananchi na taifa kwa ujumla.

TAKUKURU YANUSURU MAMILIONI YA FEDHA ZA UMMA

Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) mkoani Geita imefanikiwa kuzuia upotevu wa zaidi ya Sh milioni 94.21 zilizokuwa zimefujwa kupitia miradi ya maendeleo na malipo haramu.

MHE.AYOUB AWASILISHA BAJETI YA MAMBO YA NDANI 2026 /2027

Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Ayoub Mohammed Mahmoud, amewasilisha Taarifa ya Randama ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Bajeti ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kwa mwaka wa fedha 2026/2027 mbele ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama (NUU)

WASIRA AWEKA JIWE LA MSINGI JENGO LA CCM GEITA

Makamu Mwenyekiti wa CCM (Bara), Stephen Wasira, amewatahadharisha wanachama wa chama hicho kuacha tabia ya kuanzisha mivutano na uchochezi wanapokosa fursa za uteuzi au kushindwa katika kura za maoni.

Akizungumza mkoani Geita wakati wa uwekaji wa Jiwe la msingi la Jengo la Ofisi za Mkoa, Wasira amesisitiza kuwa kukosa uongozi kusitumiwe kama kigezo cha kuvuruga amani ya Chama na Taifa, kwani kufanya hivyo ni kuhatarisha usalama wa Nchi.

TANESCO LINDI YAONGEZA UWEZO WA KITUO CHA MAHUMBIKA KUKIDHI MAHITAJI YA UMEME

Kutokana na ongezeko la mahitaji ya Umeme katika Mikoa ya Lindi na Mtwara, Shirika la Umeme tanzania (TANESCO) Mkoa wa Lindi limeanzisha mradi wa kuongeza uwezo wa kituo cha kupooza umeme cha maumbika kwa kufunga transfoma yenye uwezo wa zaidi ya megawati 15 kwa gharama ya zaidi ya shilingi milioni 702.

DKT. MWIGULU AWAOMBA WATANZANIA KUENDELEA KUMUOMBEA MHE. LUKUVI

WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba amewaomba Watanzania waendelee kumuombea kwa Mwenyezi Mungu aliyekuwa Waziri Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu, marehemu William Lukuvi aliyefariki jana Machi 25, 2026 katika Hospitali ya Benjamin Mkapa, jijini Dodoma.
Akiongea kwa niaba ya Serikali nyumbani kwa marehemu Area D, jijini Dodoma leo, Alhamisi, Machi 26, 2026, Waziri Mkuu amesema: “Kwa niaba ya Serikali natoa pole kwa familia, ndugu, jamaa. Jambo hili zito, gumu kulielewa, gumu kulipokea.”

HARAKATI ZA KUKITAMBUA KISWAHILI MITANDAONI ZAANZA

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo wa Tanzania Paul Makonda, amesema Serikali imeanza mazungumzo na UNESCO pamoja na Uongozi wa Kampuni Mama inayomiliki Mitandao ya Kijamii ya Faceebok, Instagram na Whatsapp (Meta) ili lugha ya Kiswahili itambulike rasmi kwenye majukwaa ya Mitandao hiyo na kuwezesha Vijana wanaotengeneza maudhui kwa Lugha hiyo walipwe malipo makubwa kulingana na kazi zao.

Makonda ameyazungumza haya wakati wa Kongamano la 5 la Idhaa za kKswahili Duniani lililofanyika Jana Arusha.

ZRCP ELIMISHENI UMUHIMU WA MATOKEO YA TAFITI

Rais Wa Zanzibar Na Mwenyekiti Wa Baraza La Mapinduzi Dkt. Hussein Ali Mwinyi, Ameushauri Uongozi Wa Kituo Cha Tafiti Za Kiuchumi, Kijamii Na Uchambuzi Wa Sera Zanzibar –Zrcp- Kuandaa Mikutano Na Mijadala Na Wadau Ili Kuwaelimisha Kuhusu Umuhimu Wa Kutumia Matokeo Ya Tafiti Katika Utekelezaji Wa Majukumu Yao.

Ni Ziara Ya Ujumbe Wa Kituo Cha Tafiti Za Kiuchumi, Kijamii Na Uchambuzi Wa Sera Zanzibar –Zrcp- Katika Ikulu Ya Vuga Hapa Zanzibar.

Subscribe to news
 

Simplenews subscription

The subscriber's email address.
Stay informed - subscribe to our newsletter.