TANESCO LINDI YAWANASA WATU WAWILI KWA KUJIUNGANISHIA UMEME KINYUME CHA SHERIA
Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) Mkoa wa Lindi limeendesha oparesheni maalumu ya kudhibiti vitendo vya kujiunganishia umeme kiholela na kinyume cha sheria, ambapo limefanikiwa kuwakamata watu wawili wanaodaiwa kujiunganishia huduma hiyo bila kufuata taratibu.









