DKT.MWIGULU ATOA WIKI MBILI KWA WIZARA YA MAJI KUTAFUTA MKANDARASI

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Mwigulu Nchemba ameipa Wizara ya Maji Wiki mbili kuhakikisha inakamilisha utaratibu wa upatikanaji wa Mkandarasi wa Ujenzi wa Mradi wa Maji kutoka chanzo cha Ziwa Chala.

Ametoa agizo hilo wakati akizungumza na Wananchi wa Kata ya Marangu-Kitowo, Wilaya ya Rombo Mkoani Kilimanjaro baada ya kupokea taarifa za Ujenzi wa Mradi wa Maji kutoka chanzo cha Ziwa Chala, Ujenzi wa Mradi wa Barabara holili(Rotima)-tarakea(nayemi), pamoja kuweka jiwe la msingi la skuli ya sekondari stephen moshi technical. 

SHILINGI BILIONI MOJA ZIMEPATIKANA USAJILI VYOMBO VYA MOTO

Wizara Ya Fedha Na Mipango Imesema Jumla Ya Vyombo Vya Moto Kumi Na Tisa Elfu 337  Vimefanyiwa Usajili Wa Namba Mpya Unaosimamiwa Na Mamlaka Ya Mapato Zanzibar Zra.

Akijibu Suali Katika Kikao Cha Baraza La Wawakilishi Naibu Waziri Wa Fedha Na Mipango Dkt. Hamad Omar Bakari Amesema Kati Ya Vyombo Hivyo Gari Zilikuwa Kumi Na Tatu Elfu Na Sitini Na Kwa Vyombo Nyengine Ni Elfu Sita Mia 277.

Amefahamisha Kuwa Katika Uendeshaji Wa Zoezi Hilo Zaidi Ya Shilingi Bilion Moja Zimekusanywa Kwa Kipindi Cha Miezi Mitatu Tokea Zoezi Hilo Kuanza.

WAMILIKI WA HOTELI WATAKIWA KUSIMAMIA MAZINGIRA YA USAFI WA FUKWE

Meneja wa hifadhi ya Kisiwa cha Mnemba na huba ya Chwaka Ndg.Omar Hakim Foum amewasihi wamiliki wa hoteli za kitalii kushirikiana kufanya usafi maeneo ya Fukwe za Zanzibar ili kuweka haiba nzuri za fukwe na kuendelea kuwavutia Watalii.

Akizungumza baada ya kufanya usafi wa mazingira uliowashorikisha Wafanya kazi wa Hoteli huko Nungwi amesema lengo la kufanya usafi Eneo hilo ni kuona maeneo ya Fukwe yanakuwa safi ili kuendana na dhamira ya Uchumi wa Buluu.

UPATIKANAJI BIDHAA ZA FUTARI WARIDHISHA KATIKA SOKO LA MAJENGO

Wafanya Biashara wa bidhaa za Vyakula na Viungo katika Soko la Majengo Jijini Dodoma wamesema upatikanaji wa bidhaa hizo umekuwa wa kuridhisha hali inayoleta taswira nzuri ya upatikanaji wa Futari katika Kipindi cha Mfungo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani.

Wakizungumza na ZBC wamesema bidhaa nyingi tayari zimeshafikishwa Sokoni hapo ikiwemo Ndizi, Mihongo, Viazi Vitamu, Mbatata na Maharage kwa ajili ya maandalizi ya Mwezi huo.

MHE. AYOUB APIGA HATUA KUBWA KUTEKELEZA AHADI KWA VITENDO

Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi na Mbunge wa Jimbo la Chaani, Mhe. Ayoub Mohammed Mahmoud, ameendelea kuimarisha uhai wa Chama cha Mapinduzi (CCM) kwa kukamilisha ukarabati wa matawi mawili kwa kupiga plaster, huku tawi la Ketwa likiwa hatua za mwisho.

​Mhe. Ayoub alizungumza hayo katika mkutano wa hadhara wa CCM uliofanyika visiwani Zanzibar, ambapo alibainisha kutenga shilingi milioni 20 kwa ajili ya mashindano ya Qur'an ya jimbo ili kuimarisha umoja wa wananchi wa Chaani.

DKT. MWINYI ATAKA MISIKITI ITUMIKE KWA MANUFAA YA DUNIA NA AKHERA

Rais Wa Zanzibar Na Mwenyekiti Wa Baraza La Mapinduzi Alhaj Dkt. Hussein Ali Mwinyi Amewataka Wananchi Kuhakikisha Wanaitumia Misikiti Kwa Kufanya Ibada Na Taaluma Nyingine Ili Kuleta Maslahi Mapana Kwa Ujenzi Wa Maisha Ya Dunia Na Akhera.

Dk Mwinyi Ameyasema Hayo Katika Hafla Ya Ufunguzi Wa Msikiti Wa Ijumaa Chachani Wilaya Ya Chake Mkoa Wa Kusini Pemba.

Alhaj Doctor Mwinyi Amesema Misikiti Ni Mahapa Pekee Pa Kukutana Na Kujadili Masuala Yanayoikabili Jamii Ikiwemo Kuwa Saidia Mayatima Wajane Na Wasiojiweza Il Kujenga Mustakbali Mwema Wa Maisha Na Mendeleo Yao

SMZ NA SMT KUTOA ELIMU YA MUUNGANO KWA WANANCHI.

Waziri Wa Nchi Ofisi Ya Makamu Wa Pili Wa Rais Sera Uratibu Na Baraza La Wawakilishi Mhe Hamza Hassan Juma Amesema Muungano Wa Tanganyika Na Zanzibar Ndio Tunu Pekee Ya Watanzania Inayowaweka Pamoja Katika Kuimarisha Maendeleo.

Akizungumza Katika Kikao Cha Ushirikiano Baina Ya Ofisi Ya Makamu Wa Pili Wa Rais Zanzibar Na Ofisi Ya Makamu Wa Rais Tanzania Kwa Ajili Ya Kujadili Masuala Ya Muungano Na Yasiyo Ya Muungano Waziri Hamza Amesema Watanzania Wanapaswa Kuutumia Muungano Kama Ni Fursa Katika Kukuza Uchumi Ujamaa Na Ulinzi Kwa Kupitia Sekta Mbalimbali Ikiwemo Michezo.

SERIKALI ITAENDELEA KUJENGA UCHUMI JUMUISHI

Serikali Ya Mapinduzi Ya Zanzibar Itaendelea Na Azma Yake Ya Kujenga Uchumi Shindani Na Jumuishi Kwa Kuifanya Zanzibar Kuwa Sehemu Rafiki Ya Biashara Na Uwekezaji Kwa Kuweka Miundombinu Imara, Sera Bora Na Huduma Zenye Ufanisi.

RAIS SAMIA AMESISITIZA VIPAUMBELE VYENYE UMUHIMU KWA TANZANIA NA AFRIKA

Rais Wa Jamhuri Ya Muungano Watanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan Amesisitiza Vipaumbele Vyenye Umuhimu Kwa Tanzania Na Afrika Kwa Ujumla, Ikiwemo Ustahimilivu Wa Majanga, Uendelevu Wa Madeni, Mpito Wa Haki Wa Nishati Safi, Uongezaji Thamani Wa Madini Muhimu, Na Usalama Wa Chakula.

Rais Samia Ameyasema Hayo Katika Mkutano Wa 39 Wa Wakuu Wa Nchi Na Serikali Wa Umoja Wa Afrika (Au) Unaoendelea Jijini Addis Ababa Ethiopia.

MHE. AYOUB AANZA UTEKELEZAJI WA AHADI NNE ZA MAENDELEO JIMBO LA CHAANI

Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Chaani, Ayoub Mohammed Mahomud ameweka bayana dhamira yake ya kuleta mapinduzi ya kiuchumi jimboni humo kwa kutangaza kuanza kwa utekelezaji wa ahadi zake nne kuu alizozitoa wakati wa kipindi cha kampeni.

​Akizungumza leo na Wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika Kisauni, Mbunge huyo amesisitiza kuwa kipaumbele chake cha kwanza ni Usalama wa Chakula, akilenga kuhakikisha jimbo hilo linakuwa na akiba ya kutosha ya chakula isiyopungua tani 100 kila mwaka.

Subscribe to news
 

Simplenews subscription

The subscriber's email address.
Stay informed - subscribe to our newsletter.