DKT.MWIGULU ATOA WIKI MBILI KWA WIZARA YA MAJI KUTAFUTA MKANDARASI
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Mwigulu Nchemba ameipa Wizara ya Maji Wiki mbili kuhakikisha inakamilisha utaratibu wa upatikanaji wa Mkandarasi wa Ujenzi wa Mradi wa Maji kutoka chanzo cha Ziwa Chala.
Ametoa agizo hilo wakati akizungumza na Wananchi wa Kata ya Marangu-Kitowo, Wilaya ya Rombo Mkoani Kilimanjaro baada ya kupokea taarifa za Ujenzi wa Mradi wa Maji kutoka chanzo cha Ziwa Chala, Ujenzi wa Mradi wa Barabara holili(Rotima)-tarakea(nayemi), pamoja kuweka jiwe la msingi la skuli ya sekondari stephen moshi technical.









