TANESCO LINDI YAWANASA WATU WAWILI KWA KUJIUNGANISHIA UMEME KINYUME CHA SHERIA

Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) Mkoa wa Lindi limeendesha oparesheni maalumu ya kudhibiti vitendo vya kujiunganishia umeme kiholela na kinyume cha sheria, ambapo limefanikiwa kuwakamata watu wawili wanaodaiwa kujiunganishia huduma hiyo bila kufuata taratibu.

FURSA MPYA KWA VIJANA BILIONI 2 KWA WATENGENEZAJI WA MAUDHUI

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Paul Makonda, amesema Wizara imepatiwa kiasi cha TZS bilioni 2 itakayowawezesha watengenezaji wa maudhui mbalimbali mitandaoni kuimarisha kazi zao na kuwaongezea kipato kupitia majukwaa ya kidijitali.

Amesema hayo Januari 29, 2026 jijini Dodoma na kubainisha kuwa, fedha hizo zimetolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa lengo la kuyawezesha makundi yote ya watengeneza maudhui ikiwemo katika Sekta ya Utalii, Michezo, Habari, Jamii, Muziki, Filamu na sanaa nyinginezo.

SHETTA AIWAKILISHA DAR ES SALAAM KATIKA JUKWAA LA UONGOZI WA MAMEYA AFRIKA

Mstahiki Meya wa Jiji la Dar es Salaam, Nurdin Bilal Juma (Shetta), kwa sasa yupo Cape Town, Afrika Kusini, akishiriki katika mkutano wa African Mayoral Leadership Initiative (AMALI) unaowakutanisha mameya na viongozi wa miji kutoka barani Afrika.

Katika mkutano huo, Mstahiki Meya alipata fursa ya kuwasilisha maono ya urithi wa uongozi (legacy pitch) kwa niaba ya Jiji la Dar es Salaam akiweka mbele ajenda ya maendeleo jumuishi, ajira kwa vijana, na uongozi wa miji unaozingatia watu.

DKT SAMIA AZINDUA MPANGO WA KUSOMA KUANDIKA NA KUHESABU

Rais Wa Jamuhuri Ya Muungano Wa Tanzania Mh.Dk. Samia Suluhu Hassan Amezindua Mpango Mkakati Wa Sayansi Wa Kujenga Umahiri Wa Kusoma, Kuandika Na Kuhesabu (Kkk)Kwa Watoto Wa Elimu Awali Na Wanafunzi Wa Darasa La Kwanza Na La Pili.

Akizungumza Katika Uzinduzi Wa Mpango Huo Uliofanyika Jiji Dar Es Salaam, Rais SamiaAmesema Kuwa Serikali Imejidhadhati Kuhakikisha Kuwa Hakuna Mtoto Atakaye Fika Darasa La Tatu Bila Ya Kuwa Na Uwezo Wa Kusoma Kuandika, Kuandika Na Kuhesabu. 

MFUMO WA KIELEKRONI MAHAKAMANI WARAHISISHA UENDESHAJI WA KESI

Jaji Mkuu Wa Zanzibar, Khamis Ramadhani Abdalla Amesema Kuwepo Kwa Mfumo Wa Uendeshaji Wa Mashauri Kwa Njia Ya Kielektroniki Kumerahisisha Usikilizaji Wa Kesi, Na Kuchangia Upatikanaji Wa Haki Kwa Haraka.

Akizindua Mfumo Wa Majaribio Wa Uendeshaji Wa Mashauri Kwa Njia Ya Kielektroniki Huko Verde Amesema Lengo La Kuanzisha Mfumo Huo Ni Kuongeza Ufanisi Na Uwajibikaji Katika Mahkama Pamoja Na Kuondosha Urasimu Wa Haki Kwa Wananchi.

WATATU WATHIBITISHWA KUWA WENYEVITI WA BUNGE

Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania leo limewathibitisha Wabunge Deo Mnyika, Cecilia Pareso na Nagma Murtaza Giga kuwa Wenyeviti wa Bunge hilo .

Hayo yamejiri baada ya Spika wa Bunge Mussa Azzan Zungu kuwahoji Wabunge kikanuni kama waanafiki Wabunge hao kuwa Wenyeviti wa Bunge.

Wabunge hao waliteuliwa na Kamati kuu ya Chama cha Mapinduzi CCM kilichoongozwa na Mwenyekiti wa Chama hicho Dkt.Samia Suluhu Hassan January 25 Mwaka huu Mjini Zanzibar.

KILIO CHA SHERIA YA HABARI ZANZIBAR CHAIBULIWA UPYA

Wadau wa Vyombo vya Habari Nchini wameibua tena kilio chao cha kupatikana kwa sheria ya habari hapa Zanzibar na kwa kauli moja wameitaka Wizara ya Habari, Sanaa Utamaduni na Michezo kuhakikisha wanaikata kiu yao ya muda mrefu ya kuipata sheria hii.

Huu ulikuwa ni Mkutano mahususi kati ya Wizara ya Habari, Sanaa Utamaduni na Michezo na Wadau wa Sekta ya Habari ukiwa na lengo la kupata maoni, ushauri kero na mjadala wa kujenga uhuasiano mwema kati ya Sekta ya Habari na Wadau wake.

MAMA SAMIA NI KIONGOZI WA MFANO WA MAENDEELEO

Akinamama waliojifungua katika Hospital ya Wilaya Vitongoji Chake Chake Kituo cha Afya Kendwa na Tundauwa, wamesema Dkt. Samia ni Kiongozi imara na mwenye maono makubwa katika kuileta Nchi maendeleo.

Akinamama hao wameyasema hayo kwa nyakati tofauti mara baada ya kupokea zawadi kutoka  Ofisi ya CCM uratibu Pemba kwa akina mama hao

Waliyojifungua ikiwa ni kusherekea Siku ya Kuzaliwa ya Rais wa Jamuhuri ya Muungano  wa Tanzania Mama Samia Suluhu Hassan .

FUKWE YA FORODHANI SI SALAMA KWA WATOTO KUOGELEA

Kumekuwa na Ongezeko la matukio ya ajali za kuzama kwa Watoto na hata Watu Wazima mara kwa mara katika Eneo la Forodhani. Eneo hilo linatajwa kuwa na kina kirefu cha Maji na hakuna maelekezo ya Tahadhari.

Hapana shaka kwamba Eneo la Forodhani hapa Zanzibar ni moja ya Maeneo yenye Fukwe safi na haiba si tu kustarehe, lakini ile sura ya Utalii wa Zanzibar. hata hivyo baadhi ya Maeneo ya Fukwe hiii maarufu kwa sasa ni hatarishi hususani kwa Watoto kuogelea ama Mtu asiye na ujuzi wa Kuogelea.

UJENZI WA BARABARA TUNGUU-MAKUNDUCHI WAIVA

Asilimia 45 ya Vifaa vitakavyotumika kataika Ujenzi wa Barabara ya Tunguu- Makunduchi na Fumba Kisauni vimekamilika tayari kuanza Ujenzi.

Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Dkt. Khalid Salum Muhamed amekagua Kambi ya Mecco, Kampuni inayojenga Barabara hizo nakueleza kuridhishwa kwake na matayarisho yalifofanyika.

Hii si Biashara ya Gari lakini ni Kambi maalum ya Ujenzi wa Barabara ya Urefu wa Kilomita 48 ya Tunguu-Makunduchi na Barabara ya Fumba Kisauni yenye Urefu wa Kilomita 12.

Subscribe to news
 

Simplenews subscription

The subscriber's email address.
Stay informed - subscribe to our newsletter.