VIONGOZI WAHAMASISHWA KUWASAIDIA WANANCHI

Makamu Wa Pili Wa Rais Wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla Amewahamasisha Viongozi Kuwasaidia Wananchi Hasa Katika Kipindi Cha Mwezi Mtukufu Wa Ramadhani Ili Kuweza Kuweka Uwiano Sawa Wa Mahitaji.

Mhe. Hemed Ambae Ni Mwakilishi Wa Jimbo La Kiwani, Ametoa Wito Huo Baada Ya Ugawaji Wa Futari Kwa Wananchi Wa Jimbo Hilo Shehia Ya Kendwa Yenye Nyumba Zaidi Ya 1156 Hafla Iliyofanyika Kwenye Uwanja Wa Mpira Wa Mauwanifutari Kwa Wananchi Wote Hasa Wenye Mahitaji Maalum.

SERIKALI ITAENDELEA KUJENGA UCHUMI JUMUISHI

Serikali Ya Mapinduzi Ya Zanzibar Itaendelea Na Azma Yake Ya Kujenga Uchumi Shindani Na Jumuishi Kwa Kuifanya Zanzibar Kuwa Sehemu Rafiki Ya Biashara Na Uwekezaji Kwa Kuweka Miundombinu Imara, Sera Bora Na Huduma Zenye Ufanisi.

JAPAN NA ZANZIBAR ZAAHIDI KUSHIRIKIANA

Makamu Wa Pili Wa Rais Wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla Amesema Serikali Ya Mapinduzi Ya Zanzibar Itaendeleza Uhusiano Ulipo Kati Ya Serikali Ya Japan Na Zanzibar Uliodumu Kwa Muda Mrefu.

Mhe. Hemed Ameyasema Hayo Alipofanya Mazungumzo Na Balozi Wa Japan Nchini Tanzania Yoichi Mikami Afisini Kwake Vuga Zanzibar.

Amesema Uhusiano Uliopo Kati Ya Tanzania Na Japan Utaendelea Kukuza Ushirikiano Katika Pande Zote Mbili Katika Kuimarisha Sekta Za Kilimo, Biashara, Maji Safi Na Salama, Maendeleo Ya Viwanda, Utalii Na Miundombinu Mbali Mbali.

Subscribe to MAKAMU WA PILI WA RAIS ZANZIBAR
 

Simplenews subscription

The subscriber's email address.
Stay informed - subscribe to our newsletter.