ZANZIBAR YAKABILIWA NA UHABA WA WATAALAMU WA USONJI
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amesema hali ya Usonji kwa Watoto ni changamoto kubwa katika Jamii, hivyo Serikali ina wajibu wa kuhakikisha inaunga mkono jitihada za kuwasaidia Watoto wanaoathirika na hali hiyo.
