MKUU WA MKOA WA PWANI, RC KUNENGE ASHIRIKI ZOEZI LA KUPANDA MITI

Mkuu wa Mkoa wa Pwani Alhaji Abubakari  Kunenge.
English

Katika kusheherekea sikukuu ya kuzaliwa kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan, Mkuu wa Mkoa wa Pwani Alhaji Abubakari  Kunenge ameshiriki zoezi la upandaji wa miti katika shule ya Msingi Chumbi 'A' Wilayani Rufiji Mkoani Pwani.

Zoezi hilo ni sehemu ya hatua ya kumuunga mkono Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa uamuzi wake wa kizalendo wa kuadhimisha siku yake ya kuzaliwa kwa vitendo vya kutunza mazingira kwa kupandamiti, ambapo upandaji huo wa miti ni sehemu ya upadaji miti mil.13 na laki 5 katika Halmashauri tisa zinazounganisha wilaya saba za mkoa wa Pwani.

Halmashauri zote za Mkoa wa pwani tunaenda kupanda miti  milioni 13.5 ambapo kila halmashauri itatakiwa kupanda miti milioni 1.5 baada ya zoezi hilo  tunaenda kuzindua ugawaji wa miche mili 1.5 ya mikorosho nayo itaanza kupandwa leo na zoezi hilo litaendelea. La muhimu  ni kwamba tumepanda miti kinachofuata ni kuitunza na ni  kumbukumbu nzuri, hata tukiona miti hii tunakumbuka kwamba imepandwa katika kumbukizi ya kuzaliwa kwa Rais wetu" Alisema RC Kunenge.

Zoezi hilo la upandaji wa miti lilienda sambamba na zoezi la uzinduzi ugawaji wa Miche ya miti ya Korosho mil 1.5,   kwa wakulima wa wilaya ya Rufiji katika kwa lengo la kukuza uchumi  wa mkulima mmoja mmoja wilayani humo kupitia Sekta  ya Kilimo. Kaimu Mkurugenzi wa Bodi ya Korosho Nchini CPA.Reuben Putaputa  Putaputa amesema bodi ya korosho imejiwekea Mkakati katika mikoa minne hapa nchini, yaani mkoa wa Pwani,  Lindi, Mtwara na Mkoa wa Ruvuma ajitaja kipaumbele ikiwa  ni ufufuaji wa Mashamba poli.

 

Simplenews subscription

The subscriber's email address.
Stay informed - subscribe to our newsletter.