ZANZIBAR YAJITANGAZA KIUTALII LONDON

 Kwa mara ya kwanza katika historia ya Zanzibar imezindua Matangazo ya Utalii katika Jiji la London Nchini Uingereza kwa kubandika Matangazo yanayosomeka Tembelea Zanzibar kwenye Mabasi maarufu ya Abiria yanayoitwa London Buses.    Hatimaye historia imeandikwa.

 Mabango makubwa yanayochagiza, kushajihisha na kuuvutia Utalii wa Zanzibar yameanza kuonekana Leo kwenye Mabasi ya Abira maarufu kama London Luses Nchini Uingereza.

WANASWA KWA KUHUJUMU MRADI WA MAJI WA MIJI 28

WATU wanne wamekamatwa na Jeshi la Polisi Mkoani Tabora kwa tuhuma za kuhujumu Mradi wa Maji wa Miji 28 unaoendelea kutekelezwa na serikali katika Wilaya za Sikonge, Urambo na Kaliua ili kumaliza kero ya wananchi.

Kaimu Kamanda wa Polisi ACP Constatine Mbogambi amethibitisha kukamatwa watuhumiwa hao wakiwa na vifaa mbalimbali vilivyoibiwa kwenye mradi huo Wilayani Urambo. Akitaja baadhi ya vifaa vilivyokamatwa kuwa ni mashine kubwa 3 za kuchomelea mabomba, grenda mashine 2 za kukatia mabomba, nyaya 9 za kuunganishia grenda hizo na lita 40 za mafuta ya mitambo ya hydroliki.

WATENDAJI KITUO CHA UOKOZI MWANZA WATAKIWA KUTOA HUDUMA ZA DHARURA KWA SAA 24

WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba, ametoa maagizo kwa watendaji wa Kituo cha Kuratibu. Utafutaji na Uokozi cha Kikanda – Mwanza, chenye thamani ya takribani shilingi bilioni 19.8, kuhakikisha kituo hicho kinaendeshwa kwa saa 24 na kwa ufanisi wa hali ya juu.

Amesema hayo leo Januari 23, 2026 baada ya kutembelea kituo cha Kuratibu Utafutaji na Uokozi, jijini Mwanza. Huku akisisitiza kuwa huduma za uokozi ni kazi ya kuokoa maisha, hivyo hakuna uvumilivu kwa uzembe, kuchelewesha utoaji wa huduma za msaada pindi inapohitajika.

JELA MAISHA AKITUHUMIWA KULAWITI MWANAFUNZI WA MIAKA MITANO

Mkazi mmoja wa kata ya Mkata  wilaya ya Handeni Mkoani Tanga Said Mbezi (23) amehukumiwa kifo cha maisha jela baada ya kukutwa na hatia ya kumlawiti mtoto wa miaka mitano.

Hukumu hiyo imetolewa Jumatano Januari 21,2026 na Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya wilaya ya Pangani  Fransisca Magwiza baada ya kuridhishwa na ushahidi uliotolewa  mahakamani hapo.

Awali ilielezwa mahakamani hapo kuwa mtuhumiwa alitenda kosa hilo mnamo Oktoba 15,2024 katika kijiji cha Mkwaja wilaya ya Pangani kwa kumlawiti kijana wa miaka mitano ambae ni mwanafunzi wa darasa la awali.

SERIKALI INAENDELEA KUWEKEZA KWENYE MIUNDOMBINU YA SEKTA YA ELIMU

Rais wa Zanzibar na mwenyekiti wa baraza la Mapinduzi Dkt. Hussein Ali Mwinyi amesema Serikali inaendelea kuwekeza kwenye miundombinu ya sekta ya elimu ili kuwawezesha vijana kusoma fani tofauti ndani ya Nchi.

 Rais wa Zanzibar ameyasema hayo katika mahafali ya 19 ya Chuo kikuu cha Taifa cha Zanzibar SUZA na kuwatunuku vyeti, stashahada, shahada, shahada za uzamili na uzamivu kwa wahitimu wa Chuo hicho kwa mwaka wa masomo 2022/2023, huko Tunguu Mkoa wa Kusini Unguja.

DK. SHEIN AMEITAKA SERIKALI YA ZANZIBAR KUWASOMESHA WAFANYAKAZI WA KADA MBALIMBALI

Rais Mstahafu wa awamu ya saba wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Dk. Ali Mohamed Shein ameitaka Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kuwasomesha wafanyakazi wa kada mbalimbali wakiwemo wa afya ili waweze kutoa huduma bora kwa Wananachi.

Ameyasema hayo mbuzini wilaya ya magharib a katika ufunguzi wa Hospitali ya wilaya ikiwa ni shamra shamra ya maadhimisho ya miaka 60 ya Mapinduzi Zanzibar.

Rais wa Tanzania Dr. Samia Suluhu Hassan afupisha safari yake Dubai

Rais wa Tanzania Dr. Samia Suluhu Hassan ambaye amekuwepo Dubai kwa ajili ya Mkutano wa Umoja wa Mataifa wa Mabadiliko ya Tabianchi (COP28), ameamua kufupisha safari hiyo na kurejea nchini haraka iwezekanavyo ili kushughulikia kwa karibu janga la mafuriko Wilayani Hanang ambalo limesababisha vifo vya zaidi ya Watu 50 na zaidi ya 80 kujeruhiwa.

Habari kubwa Magazetini Kenya leo December 5, 2023

Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania December 5. 2023,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za nyuma Magazetini kenya.

Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu kurejelea kesi yake na tuhuma za ufisadi

Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu anatazamiwa kurejea kwa kesi yake ya muda mrefu ya tuhuma nyingi za ufisadi, baada ya kusimama kwa sababu ya vita huko Gaza.

Mahakama mjini Jerusalem inatazamiwa kuanza kusikiliza kesi hiyo, ambayo inaangazia mashtaka kadhaa ya ufisadi dhidi ya Netanyahu, siku ya Jumatatu, kulingana na ripoti katika vyombo vya habari vya Israel. Kesi hiyo ilisitishwa kwa amri ya dharura kutoka kwa waziri wa sheria wa nchi hiyo kufuatia shambulio la Hamas dhidi ya Israel tarehe 7 Oktoba.

Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete wametembelea skuli ya Maandalizi ya Awali ya Kikaangoni Wilaya ya Maagharibi

Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Shirika la Ushirikiano wa Elimu Duniani (GPE), Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na Makamu Mwenyekiti wake Bi.Susan Liautaud kulia wametembelea skuli ya Maandalizi ya Awali ya Kikaangoni Wilaya ya Maagharibi.

Subscribe to news
 

Simplenews subscription

The subscriber's email address.
Stay informed - subscribe to our newsletter.