SERIKALI KUTUMIA BILIONI 79 KUJENGA VITUO VYA POLISI 698 NCHI NZIMA

Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Ayoub Mohammed Mahmoud, amesema Serikali imepanga kutumia zaidi ya Shilingi Bilioni 79 kwa ajili ya ujenzi wa vituo vya polisi 698 nchini, ikiwa ni mkakati wa kuimarisha usalama wa raia na mali zao.

​Akizungumza leo wakati wa ziara yake ya kukagua miradi ya Vituo vya Jeshi la Polisi visiwani Zanzibar Mhe. Ayoub Mahmoud amebainisha kuwa uamuzi huo umekuja baada ya Serikali kuona kuna uhitaji wa kusogeza huduma za Kipolisi karibu na wananchi zaidi.

MHE. AYOUB APIGA HATUA KUBWA KUTEKELEZA AHADI KWA VITENDO

Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi na Mbunge wa Jimbo la Chaani, Mhe. Ayoub Mohammed Mahmoud, ameendelea kuimarisha uhai wa Chama cha Mapinduzi (CCM) kwa kukamilisha ukarabati wa matawi mawili kwa kupiga plaster, huku tawi la Ketwa likiwa hatua za mwisho.

​Mhe. Ayoub alizungumza hayo katika mkutano wa hadhara wa CCM uliofanyika visiwani Zanzibar, ambapo alibainisha kutenga shilingi milioni 20 kwa ajili ya mashindano ya Qur'an ya jimbo ili kuimarisha umoja wa wananchi wa Chaani.

MHE. AYOUB AANZA UTEKELEZAJI WA AHADI NNE ZA MAENDELEO JIMBO LA CHAANI

Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Chaani, Ayoub Mohammed Mahomud ameweka bayana dhamira yake ya kuleta mapinduzi ya kiuchumi jimboni humo kwa kutangaza kuanza kwa utekelezaji wa ahadi zake nne kuu alizozitoa wakati wa kipindi cha kampeni.

​Akizungumza leo na Wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika Kisauni, Mbunge huyo amesisitiza kuwa kipaumbele chake cha kwanza ni Usalama wa Chakula, akilenga kuhakikisha jimbo hilo linakuwa na akiba ya kutosha ya chakula isiyopungua tani 100 kila mwaka.

HATUJAANGUSHA NDEGE NI ZOEZI LA UTAYARI (ZAA)

Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Zanzibar (ZAA) imefanya zoezi la utayari ikiwa ni sehemu ya majukumu yake ya kawaida ya usalama wa anga katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume (AAKIA), lenye lengo la kupima uwezo wa kukabiliana na matukio ya dharura yanayoweza kutokea katika Viwanja vya Ndege.

ZANZIBAR YAJIANDAA NA DHARURA ZA NDEGE

Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Zanzibar imefanikiwa kutekeleza zoezi la kujiandaa na kukabiliana na dharura za Ndege, hatua inayolenga kuimarisha uratibu kati ya Taasisi za Ulinzi, usalama na usimamizi wa maafa.  Zoezi hilo limefanyika katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa Abeid Amani Karume 

Hayo yamebainishwa na Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Zanzibar Mulhat Yussuf Said wakati akizungumza na Waandishi wa Haaabari 

Subscribe to ZANZIBAR
 

Simplenews subscription

The subscriber's email address.
Stay informed - subscribe to our newsletter.