HATUJAANGUSHA NDEGE NI ZOEZI LA UTAYARI (ZAA)
Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Zanzibar (ZAA) imefanya zoezi la utayari ikiwa ni sehemu ya majukumu yake ya kawaida ya usalama wa anga katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume (AAKIA), lenye lengo la kupima uwezo wa kukabiliana na matukio ya dharura yanayoweza kutokea katika Viwanja vya Ndege.

