WIZARA YA AFYA YAFUATILIA MATIBABU YA KIJANA ALIEUMIA KWENYE MAKACHU

Kaimu Waziri Wa Afya Zanzibar Na Waziri Wa Nchi Afisi Ya Raisi Ikulu Dkt. Saada Mkuya Salum,Amesema Serikali Kupitia Wizara Ya Afya Itaendelea Kusimamia Matibabu Ya Abdallah Bakari Aliepata Ajali Ya Kupooza Mwili Ili Kuona Anarudi Katika Hali Yake Ya Kawaida.

Akizungumza Wakati Alipomtembelea Kijana Huyo Na Kuangalia Maendeleo Yake Huko Nyumbani Kwao Jang’ombe,Dkt.Saada Amesema Tokea Kutokea Kwa Ajali Hiyo Serikali Imekuwa Ikichukua Hatua Stahiki Ili Kuona Matibabu Ya Kijana Huyo Yanakwenda Kama Yanavyoelekezwa Na Wataalamu.

DKT. MKUYA ATAKA WACHUKULIWE HATUA WAHUDUMU WASIOWASIJIBIKA

Kaimu Waziri Wa Afya Zanzibar Na Waziri Wa Nchi Afisi Ya Raisi Ikulu Dkt Saada Mkuya Salum Amewataka Madaktari Dhamana Ngazi Ya Wilaya Kufanya Kazi Kwa Weledi Ili Sekta Ya Afya Ieandane Na Uwekezaji Uliofanywa Na Serikali.

Akizungumza Katika Mkutano Maalumu Na Viongozi Wa Wizara Ya Afya Pamoja Na Madaktari Hao Dkt. Saada Amesema Kwa Sasa Wananchi Wamekuwa Wakilalamikia Juu Ya Huduma Wanazozipata Katika Vituo Vya Afya Pamoja Na Hospitali, Jambo Ambalo Limekuwa Likiongeza Matatizo Kwa Wagonjwa Wanaofuata Huduma Katika Hospitali Hizo.

Subscribe to WAZIRI WA NCHI AFISI YA RAIS IKULU
 

Simplenews subscription

The subscriber's email address.
Stay informed - subscribe to our newsletter.