WIZARA YA AFYA YAFUATILIA MATIBABU YA KIJANA ALIEUMIA KWENYE MAKACHU
Kaimu Waziri Wa Afya Zanzibar Na Waziri Wa Nchi Afisi Ya Raisi Ikulu Dkt. Saada Mkuya Salum,Amesema Serikali Kupitia Wizara Ya Afya Itaendelea Kusimamia Matibabu Ya Abdallah Bakari Aliepata Ajali Ya Kupooza Mwili Ili Kuona Anarudi Katika Hali Yake Ya Kawaida.
Akizungumza Wakati Alipomtembelea Kijana Huyo Na Kuangalia Maendeleo Yake Huko Nyumbani Kwao Jang’ombe,Dkt.Saada Amesema Tokea Kutokea Kwa Ajali Hiyo Serikali Imekuwa Ikichukua Hatua Stahiki Ili Kuona Matibabu Ya Kijana Huyo Yanakwenda Kama Yanavyoelekezwa Na Wataalamu.

