AJALI YA BASI NA LORI YAUA MMOJA NA KUJERUHI 12 SHINYANGA
Basi la Kampuni ya Kisire limegongana uso kwa uso na lori katika eneo la mnada wa Tinde Wilaya ya Shinyanga na kusababisha kifo cha mtu mmoja huku wengine 12 wakijeruhiwa na kukimbizwa Kituo cha afya Tinde kupata matibabu.
Ajali hiyo imehusisha basi la Kisire lenye namba za usajili T 229 EEL, lililokuwa likitoka Kahama kuelekea Mwanza, kugongana uso kwa uso na lori la mizigo lenye namba za usajili RAE 849N. lililokuwa limebeba shehena ya mchele kutoka Dar es Salaam kwenda nchi jirani ya Rwanda huku chanzo kikielezwa kuwa ni mwendo kasi.
