DKT.SAMIA AWATAKA WATANZANIA KUJENGA UTAMADUNI WA KULINDA MAZINGIRA
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan Ametoa wito kwa Watanzania kuendelea kujenga utamaduni wa kulinda na kuhifadhi mazingira kwa hiari wakitambua kuwa ulinzi wa mazingira ni msingi wa uhai, maendeleo na usalama wa Taifa.
Rais Samia ameongoza mchakato wa upandaji miti katika Maeneo ya Bungi kilimo pamoja na Kizimkazi ikiwa ni kuadhimisha Siku yake ya Kuzaliwa ambapo amesisitiza Watanzania kuimarisha uoto wa asili na kuchangia kwa vitendo juhudi za kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabia Nchi kwa ustawi wa Maendeleo ya Taifa.
