MAFUNZO YA UTUMISHI KWA WAFANYAKAZI NI MUHIMU KAZINI
Kaimu Mkurugenzi wa Kampuni inayotoa huduma za bima zinazozingatia misingi na sharia ZIC Takaful Ndg.Said Abdallah Basleym amesema suala la Mafunzo kwa Wafanyakazi ni jambo la kupewa kipaumbele ili kuhakikisha wanaendana na kasi ya utendaji na kufanya kazi kwa ufanisi zaidi.
Akizungumza wakati wa Mafunzo ya kujenga uwezo yaliyotolewa kwa Wafanyakazi wa Kampuni hiyo, Ndg. Said ameeleza kuwa uwekezaji katika Mafunzo husaidia kuongeza ufanisi katika utendaji kazi wa Kampuni, pamoja na kuboresha huduma zinazotolewa kwa Wananchi.
