BANDARI YA MPIGADURI YAFANYA MAJARIBIO KUSHUSHA MIZIGO
Waziri Wa Ujenzi Na Uchukuzi Zanzibar, Dkt. Khalid Salum Mohamed, Amezindua Majaribio Ya Ushushaji Wa Mizigo Katika Bandari Ya Mpigaduri, Zoezi Lililofanywa Na Meli Za Kampuni Ya Azam Marine.
Akizungumza Wakati Wa Uzinduzi Huo Uliofanyika Waziri Wa Ujenzi Na Uchukuzi Ameeleza Kuridhishwa Na Majaribio Hayo, Huku Akisema Ni Sehemu Ya Jitihada Za Serikali Ya Mapinduzi Ya Zanzibar Kupunguza Msongamano Katika Bandari Ya Malindi.
Amesema Kazi Rasmi La Ushushaji Mizigo Inatarajiwa Kuanza Mwezi Aprili Mwaka Huu Baada Ya Kukamilika Kwa Majaribio Ya Awali.
