KILIO CHA SHERIA YA HABARI ZANZIBAR CHAIBULIWA UPYA
Wadau wa Vyombo vya Habari Nchini wameibua tena kilio chao cha kupatikana kwa sheria ya habari hapa Zanzibar na kwa kauli moja wameitaka Wizara ya Habari, Sanaa Utamaduni na Michezo kuhakikisha wanaikata kiu yao ya muda mrefu ya kuipata sheria hii.
Huu ulikuwa ni Mkutano mahususi kati ya Wizara ya Habari, Sanaa Utamaduni na Michezo na Wadau wa Sekta ya Habari ukiwa na lengo la kupata maoni, ushauri kero na mjadala wa kujenga uhuasiano mwema kati ya Sekta ya Habari na Wadau wake.
