ZANZIBAR YAJIANDAA NA DHARURA ZA NDEGE
Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Zanzibar imefanikiwa kutekeleza zoezi la kujiandaa na kukabiliana na dharura za Ndege, hatua inayolenga kuimarisha uratibu kati ya Taasisi za Ulinzi, usalama na usimamizi wa maafa. Zoezi hilo limefanyika katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa Abeid Amani Karume
Hayo yamebainishwa na Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Zanzibar Mulhat Yussuf Said wakati akizungumza na Waandishi wa Haaabari

