WANAWAKE WAHIMIZWA KUSIMAMIA MALEZI
Baada ya kufanikiwa kiuchumi Wanawake Nchini wameaswa kuzingatia mila na desturi zinazojenga na sio kubomoa na kuharibu kizazi cha baadae
Kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani Mkoani Geita kilopambwa na ujumbe mzito wa kuwataka Wanawake Nchini kuoanisha mafanikio ya kiuchumi na utunzaji wa mila na desturi bora.
Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi maalum, Dkt. Dorothy Gwajima, amesisitiza kuwa juhudi za Serikali za kumuinua Mwanamke kiuchumi hazina lengo la kubomoa misingi ya Familia, bali ni kupunguza ukatili Majumbani.
