MADIWANI MBULU WATAKA WASIOCHANGIA CHAKULA SHULENI WACHUKULIWE HATUA

Baraza la madiwani wa halmashauri ya mji wa Mbulu mkoani Manyara wameiomba Serikali  kuwachukulia hatua kali za kisheria Wazazi wasiochangia chakula kwa watoto wao shuleni ili kuwezesha watoto kupata chakula cha mchana na kuinua kiwango cha taaluma.


Madiwani hao Wametoa Ombi hilo wakati wa kikao cha kwanza cha baraza hilo ambapo wamelalamikia tabia ya baadhi ya wazazi kutochangia mchango wa chakula shuleni kwa watoto wao hali inayokuwa kikwazo kwa jitihada za kuinua taaluma na kuondokana na utoro shuleni.

Subscribe to Manyara Tanzania
 

Simplenews subscription

The subscriber's email address.
Stay informed - subscribe to our newsletter.