FUKWE YA FORODHANI SI SALAMA KWA WATOTO KUOGELEA
Kumekuwa na Ongezeko la matukio ya ajali za kuzama kwa Watoto na hata Watu Wazima mara kwa mara katika Eneo la Forodhani. Eneo hilo linatajwa kuwa na kina kirefu cha Maji na hakuna maelekezo ya Tahadhari.
Hapana shaka kwamba Eneo la Forodhani hapa Zanzibar ni moja ya Maeneo yenye Fukwe safi na haiba si tu kustarehe, lakini ile sura ya Utalii wa Zanzibar. hata hivyo baadhi ya Maeneo ya Fukwe hiii maarufu kwa sasa ni hatarishi hususani kwa Watoto kuogelea ama Mtu asiye na ujuzi wa Kuogelea.
