DKT. MWINYI ATEMBELEA MJI WA AFCON FUMBA
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Ali Mwinyi, ameutembelea mradi wa Mji wa Afcon Fumba uliopo Mkoa wa Mjini Magharibi.
Katika Ziara hiyo Dkt. Mwinyi amembatana na Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Dkt. Riziki Pembe Juma, pamoja na Wadau wa Mradi wa Afcon Fumba Zanzibar.
