POLISI WANAWAKE MKOA WA ARUSHA WAMETAKIWA KUJIEPUSHA NA VITENDO VINAVYOKWENDA KINYUME JESHI HILO
Katibu wa Mtandao wa Polisi Wanawake Tanzania TPF net Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi SACP Pili Mande amewataka Askari wa kike Mkoa wa Arusha kujiepusha na vitendo ambavyo ni kinyume na maadili ya Jeshi hilo.
Kauli hiyo ameitoa leo wakati akitoa mafunzo yaliyoandaliwa na mtandao huo kutoka makao makuu ya Jeshi la Polisi kwa ajili ya kuwajengea uwezo Askari wa kike Jijini humo ambapo amewataka kutambua malengo mazuri ya kuanzishwa kwa mtandao huo.