SERIKALI INAENDELEA KUWEKEZA KWENYE MIUNDOMBINU YA SEKTA YA ELIMU

Rais wa Zanzibar na mwenyekiti wa baraza la Mapinduzi Dkt. Hussein Ali Mwinyi amesema Serikali inaendelea kuwekeza kwenye miundombinu ya sekta ya elimu ili kuwawezesha vijana kusoma fani tofauti ndani ya Nchi.

 Rais wa Zanzibar ameyasema hayo katika mahafali ya 19 ya Chuo kikuu cha Taifa cha Zanzibar SUZA na kuwatunuku vyeti, stashahada, shahada, shahada za uzamili na uzamivu kwa wahitimu wa Chuo hicho kwa mwaka wa masomo 2022/2023, huko Tunguu Mkoa wa Kusini Unguja.

DK. SHEIN AMEITAKA SERIKALI YA ZANZIBAR KUWASOMESHA WAFANYAKAZI WA KADA MBALIMBALI

Rais Mstahafu wa awamu ya saba wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Dk. Ali Mohamed Shein ameitaka Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kuwasomesha wafanyakazi wa kada mbalimbali wakiwemo wa afya ili waweze kutoa huduma bora kwa Wananachi.

Ameyasema hayo mbuzini wilaya ya magharib a katika ufunguzi wa Hospitali ya wilaya ikiwa ni shamra shamra ya maadhimisho ya miaka 60 ya Mapinduzi Zanzibar.

Rais wa Tanzania Dr. Samia Suluhu Hassan afupisha safari yake Dubai

Rais wa Tanzania Dr. Samia Suluhu Hassan ambaye amekuwepo Dubai kwa ajili ya Mkutano wa Umoja wa Mataifa wa Mabadiliko ya Tabianchi (COP28), ameamua kufupisha safari hiyo na kurejea nchini haraka iwezekanavyo ili kushughulikia kwa karibu janga la mafuriko Wilayani Hanang ambalo limesababisha vifo vya zaidi ya Watu 50 na zaidi ya 80 kujeruhiwa.

Habari kubwa Magazetini Kenya leo December 5, 2023

Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania December 5. 2023,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za nyuma Magazetini kenya.

Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu kurejelea kesi yake na tuhuma za ufisadi

Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu anatazamiwa kurejea kwa kesi yake ya muda mrefu ya tuhuma nyingi za ufisadi, baada ya kusimama kwa sababu ya vita huko Gaza.

Mahakama mjini Jerusalem inatazamiwa kuanza kusikiliza kesi hiyo, ambayo inaangazia mashtaka kadhaa ya ufisadi dhidi ya Netanyahu, siku ya Jumatatu, kulingana na ripoti katika vyombo vya habari vya Israel. Kesi hiyo ilisitishwa kwa amri ya dharura kutoka kwa waziri wa sheria wa nchi hiyo kufuatia shambulio la Hamas dhidi ya Israel tarehe 7 Oktoba.

Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete wametembelea skuli ya Maandalizi ya Awali ya Kikaangoni Wilaya ya Maagharibi

Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Shirika la Ushirikiano wa Elimu Duniani (GPE), Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na Makamu Mwenyekiti wake Bi.Susan Liautaud kulia wametembelea skuli ya Maandalizi ya Awali ya Kikaangoni Wilaya ya Maagharibi.

MAUAJI YA BILIONEA MSUYA: Niliona wakimpiga risasi, kutoroka na bodaboda-2

Agosti 7, 2023 jiji la Arusha na miji ya Moshi na Mirerani ilitikiswa na taarifa za kuuawa kwa kupigwa kwa risasi, mfanyabiashara maarufu wa madini, Erasto Msuya maarufu kwa jina la Bilionea...

Subscribe to news
 

Simplenews subscription

The subscriber's email address.
Stay informed - subscribe to our newsletter.