Man U wanachunguzwa kwa kuwapa mashabiki nyama mbichi ya kuku

Manchester United inachunguzwa na Baraza la Trafford kufuatia madai kwamba mashabiki walilishwa nyama ya kuku mbichi katika hafla iliyoandaliwa hivi majuzi huko Old Trafford.

Watu kadhaa wanadai kuwa hawakuwa sawa kufuatia tukio hilo na tukio hilo sasa linachunguzwa.

Kwa mujibu wa gazeti la Athletic, United ilipokea malalamiko kadhaa na wanafanya uchunguzi wao wa ndani

Klabu inapata mapato makubwa kutokana na kuhudumia chakula na kuandaa hafla na kupunguzwa kwa viwango vyao vya usafi kunaweza kuathiri hilo.

klabu ya Man United ni suala la wachezaji wake kuchelewa mazoezini

Kiungo wa zamani wa Manchester United na Chelsea, Nemanja Matiç raia wa Serbia amesema kuwa moja ya kitu kipya alichokutana nacho alipojiunga na klabu ya Man United ni suala la wachezaji wake kuchelewa mazoezini.

Matic ameeleza kuwa wakati akiwa Chelsea wachezaji wote walikuwa professional na walikuwa wakifika mazoezini kwa wakati lakini United ilikuwa tofauti licha ya kuwekwa adhabu ya faini kwa wale wanaochelewa.

Subscribe to manchesta
 

Simplenews subscription

The subscriber's email address.
Stay informed - subscribe to our newsletter.